Sudan, Djibouti zaondolewa Afcon U17 kisa umri

Imethibitishwa kuwa mataifa mawili ya Afrika yameondolewa katika mashindano ya vijana baada ya kugundulika kuwa yalikuwa yakidanganya umri.
Udanganyifu wa umri umekuwa jambo la kawaida katika bara la Afrika kwa miaka mingi, na kwa bahati mbaya limejirudia kwa mara nyingine tena, wakati huu katika mechi za kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Vijana chini ya umri wa miaka 17.
Kwa mujibu wa BBC Sport, Sudan na Djibouti zimefuzu katika michuano hiyo baada ya Baraza la Vyama vya Soka vya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kugundua kuwa mataifa hayo yaliyotajwa yalikuwa yanatumia wachezaji waliozidi umri.
Baraza tawala la eneo lilitumia picha ya sumaku (MRI) kukagua vifundo vya mikono ya wachezaji ili kubaini usahihi wa umri wao kabla ya mechi za mchujo kuanza katika mji mkuu wa Ethiopia wa Addis Ababa.
Kutokana na kuondolewa kwa Sudan na Djibouti, waliofuzu kikanda sasa wana washiriki sita pekee. Makundi yalipangwa upya kufuatia kuondoka kwa mataifa hayo, huku wenyeji Ethiopia, Tanzania na Somalia wakimenyana katika Kundi A, huku Kundi B linaundwa na Uganda, Burundi na Sudan Kusini.
Washindi wa fainali za michuano hiyo watawakilisha CECAFA katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 nchini Algeria 2023.