Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Srelio haitaki kurudia makosa

SCELIO Pict

Muktasari:

  • Ligi hiyo ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL), itaendelea kesho Jumamosi kwa michezo minane itakayochezwa kwenye Uwanja wa Donbosco Upanga unaotumika.

BAADA ya timu ya Srelio kupoteza michezo miwili ya kwanza, kocha wa timu hiyo Miyasi Nyamoko amesema kwa mechi dhidi ya maafande wa ABC hawatarudia makosa katika vita ya Ligi ya Kikapu ya Mkoa wa Dar es Salaam (BDL).

“Kwa kweli hadi tunafikia michezo tulizopoteza, tumeitana na tumejadiliana, ili kujua kitu kilichotungusha na tumeshajua sababu na sasa tunarudi kivingine,” alisema Nyamoko.

Hata hivyo, kufanya vibaya katika  michezo hiyo, imeonyesha ni kutokana na kutokuwepo kwa wachezaji  watatu wa kimataifa akiwamo  Sponican Ngoma, Joseph Kamamba (Zambia) na Chaly Kasseng (Cameroun).

Srelio ilifungwa na Mchenga Star kwa pointi 82-70 kisha kulala kwa Dar City kwa pointi 105-32

Michezo mingine itakayochezwa leo upande wanawake ni kati ya DB Lioness na Mgulani JKT, Twalipo Queens na Real Dream na upande wanaume itakuwa kati ya Chui na Pazi.

Ligi hiyo ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL), itaendelea kesho Jumamosi kwa michezo minane itakayochezwa kwenye Uwanja wa Donbosco Upanga unaotumika.