Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Siri imefichuka… Kilichombakisha Diarra hiki hapa

DIARRA Pict

Muktasari:

  • Uamuzi wa Diarra kubaki Yanga umewafurahisha mashabiki wa timu hiyo, lakini kuna siri iliyojificha juu ya jambo hilo ambayo imefichuliwa na kocha raia wa Ubelgiji.

YANGA ina uhakika sasa wa kuendelea kuwa na kipa namba moja wa kikosi hicho, Djigui Diarra baada ya mwenyewe kufanya uamuzi wa kubaki ndani ya timu hiyo.

Uamuzi wa Diarra kubaki Yanga umewafurahisha mashabiki wa timu hiyo, lakini kuna siri iliyojificha juu ya jambo hilo ambayo imefichuliwa na kocha raia wa Ubelgiji.

Kocha huyo si mwingine bali ni Tom Saintfiet ambaye anamfundisha Diarra katika kikosi cha timu ya taifa ya Mali ambapo alilazimika kufanya naye kikao kilichobadili uamuzi wake.

Akizungumza na Mwanaspoti, kocha huyo alisema baada ya kusikia Diarra anataka kuondoka Yanga, alifanya naye kikao kifupi kisha akampa akili ya anachotakiwa kufanya.

Saintfiet ambaye alipita Yanga mwaka 2012 akiwaachia kombe moja la Cecafa, alisema baada ya kuona tetesi kwamba kipa huyo anataka kuondoka, amempa ushauri kwamba atulize akili kwanza kwani anaona bado yuko kwenye klabu sahihi inayopigania malengo makubwa kuliko kuhamia timu nyingine ambayo inaweza kumrudisha nyuma.

“Nilisikia Diarra anataka kuondoka Yanga, nimekutana naye na nikamsikiliza kwenye hilo, kuna mambo nimemshauri anatakiwa kuyatazama kwa akili kubwa,” alisema Saintfiet ambaye ana msimamo mkali.

“Nafahamu Diarra hawezi kukosa timu nzuri lakini timu alizonitajia zinazomtaka nadhani ni vyema akabaki Yanga kwanza kwa kuwa sioni kama sio sehemu sahihi kwake.

“Zipo timu ambazo zinaweza kukupa fedha nyingi lakini kwa hali ya vikosi vyao zinaweza kufifisha jina lake na hata kupoteza nafasi yake timu ya taifa, naona Yanga wamebadilika sana na wana njaa ya mataji makubwa ya Afrika, nadhani bado yupo sehemu sahihi.”

Diarra alikuwa anataka kutimkia Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini lakini nayo ikajiondoa kwenye mbio za kumsajili akielezwa kusalia na ofa moja ya Uarabuni.

Kipa huyo aliyetua Yanga Agosti 8, 2021 akitokea Stade Malien ya Mali, bado ana miaka miwili katika mkataba wake, na Mwanaspoti linafahamu kabla ya kujiunga na kambi ya timu ya taifa, alikutana na tajiri wa Yanga, Ghalib Said Mohammed ‘GSM’ na kukubaliana kubaki labuni hapo.