Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Simba: Manula yupo fiti kucheza

Klabu ya Simba imesema golikipa Aishi Manula amepona jeraha lake baada ya kufanyiwa upasuaji wa nyama za paja na sasa yupo fiti kucheza.

Manula aliumia katika mechi ya robo fainali ASFC dhidi ya Ihefu na amekaa nje ya uwanja kwa takribani miezi minne na tayari amefanya mazoezi na wenzake.

"Kwa sasa Manula yupo fiti kuanza kushuka dimbani kutegemea na uhitaji wa benchi la ufundi ingawa anatakiwa kuendana na kasi ya mazoezi na wenzake," imeeleza taarifa ya Simba

Simba itakuwa na kibarua cha kusaka pointi tatu kwa Tanzania Prisons kwenye mechi ya Ligi Kuu Alhamisi Oktoba 5.