Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Sababu ya Mkude kutemwa Simba yatajwa

SIMBA SC ikiendeleza kutoa 'Thank You' kwa wachezaji wake kikosini , leo imetoa tamko kuhusu kiungo Jonas Mkude aliyedumu miaka 13.

Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally kupitia akaunti yake ya Instagram ameandika kuwa muda ndiyo umetenganisha mapenzi ya timu hiyo na Mkude.

"Ameondoka mtu tunayempenda kweli, ameondoka mtoto wetu, mtoto wa nyumbani kwetu. Kwa miaka ya hivi karibuni hakuna mchezaji tumewahi kumpenda kama Jonas Mkude na tutaendelea kumpenda,"

Ahmed katika andiko hilo amedai wakati Simba ina njaa, Azam ilimuhitaji Mkude ila hakuenda, Yanga walimtaka hakuenda akachagua kuvumilia njaa na kumpongeza kuwa ni zaidi ya mchezaji.

"Sisi tulitamani Mkude amalizie mpira wake Simba kwani hatutaki kucheza nae akiwa timu nyingine,  kwa sababu tukimfunga ataumia na yeye akitufunga ataumia hatuko tayari kumuumiza Mkude wetu," ameeleza Mkude akiongeza;

"Tumetoa taarifa ya kuachana nae punde tutatoa taarifa ya kumuaga na tutamuaga kwa heshima zote
, sisi ndo tunatambua zaidi heshima ya Mkude kuliko mtu mwingine yeyote na tutamuaga kwa heshima hiyohiyo,"