Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Pablo: Hakuna pengo Simba

Simba hesabu kali

Maisha ya Bernard Morrison yamefikia mwisho ndani ya kikosi cha Simba. Kocha wa Simba, Pablo Franco amewatoa hofu mashabiki kwamba hakutakuwa na pengo lolote kikosini.

“Katika mechi na Pamba kuna Yusuph Mhilu ambaye ni mchezaji kijana na amefanya vizuri kwa kufunga mabao mawili pamoja na kutengeneza nafasi za kufunga naamini ana uwezo wa kufanya zaidi,” alisema Pablo na kuongeza;

“Wachezaji kama Kibu Denis, Pater Banda na wengineo wanaocheza kwenye nafasi hiyo naamini watafanya kazi kubwa zaidi ya wakati huu kwa kutimiza majukumu ya nafasi hiyo ili kumaliza vizuri msimu,” alisema.

Katika hatua nyingine Pablo alisema anaweza kubadili mfumo akatumia kiungo mwenye asili ya kati kwenda kucheza pembeni na mambo yakaendelea kuwa mazuri.

“Nadhani ni wakati sahihi wa kuheshimu uamuzi wa uongozi kwani Simba imesajili wachezaji wengi wenye uwezo wa wapo tayari kushindana muda wote na wana uwezo wa kuhakikisha tunashinda,” alisema Pablo na kuongeza;

“Jambo lingine zuri kwa timu kulikuwa na wachezaji wengi majeruhi ila wamerejea kama Sadio Kanoute na Taddeo Lwanga wataongeza nguvu katika kikosi.”