MKWANJA: Mastaa wa soka wanazidi kupiga pesa ndefu duniani

PARIS, UFARANSA. JARIDA la France Football limetoa orodha ya wanasoka wanaolipwa pesa nyingi duniani, huku supastaa wa Barcelona, Lionel Messi akiendelea kushika namba moja kwa mkwanja kwenye mchezo huo. Licha ya kwamba Messi hajashinda Ballon d’Or tangu 2015, staa huyo wa Argentina anavuna kiasi kikubwa cha pesa kuliko hata Cristiano Ronaldo, ambaye alishinda tuzo hiyo mwaka 2016 na 2017, wakati mshindi wa tuzo hiyo wa mwaka 2018, Luka Modric hata kwenye orodha ya wakali 20 wanaolipwa kibosi kwenye soka hayumo.
Kitu cha kushangaza, wachezaji wenzake kiungo huyo huko Real Madrid, Gareth Bale, Toni Kroos na Sergio Ramos wote wameingia kwenye orodha hii ya wanasoka 20 wanaoongoza kwa kuvuna pesa nyingi duniani. Kipato hicho kimetokana na kiasi walichovuna kupitia mishahara, bonasi na mapato ya matangazo ya kibiashara waliyofanya tangu mwa mmoja nah ii ndio orodha ya wanasoka wenye vipato vikubwa.
20. Sergio Ramos
Klabu: Real Madrid
Kipato: Dola 25.8 milioni.
19. Paul Pogba
Klabu: Manchester United
Kipato: Dola 26.1 milioni.
18. Hulk
Klabu: Shanghai SIPG
Kipato: Dola 26.2 milioni.
17. Kevin De Bruyne
Klabu: Manchester City
Kipato: Dola 26.3 milioni.
16. Sergio Aguero
Klabu: Manchester City
Kipato: Dola 27.2 milioni.
15. Oscar
Klabu: Shanghai SIPG
Kipato: Dola 27.2 milioni.
14. Kylian Mbappe
Klabu: Paris Saint-Germain
Kipato: Dola 28 milioni.
13. Mesut Ozil
Klabu: Arsenal
Kipato: Dola 28.9 milioni.
12. Toni Kroos
Klabu: Real Madrid.
Kipato: Dola 29.5 milioni.
11. Gerard Pique
Klabu: Barcelona
Kipato: Dola 30.3 milioni.
10. Luis Suarez
Klabu: Barcelona
Kipato: Dola 31.4 milioni.
9. Ezequiel Lavezzi
Klabu: Hebei China Fortune
Kipato: Dola 31.7 milioni.
8. Philippe Coutinho
Klabu: Barcelona
Kipato: Dola 33.6 milioni.
7. Alexis Sanchez
Klabu: Manchester United
Kipato: Dola 34.4 milioni.
6. Andres Iniesta
Klabu: Vissel Kobe
Kipato: Dola 37 milioni.
5. Gareth Bale
Klabu: Real Madrid
Kipato: Dola 45 milioni.
Getty
4. Antoine Griezmann
Klabu: Atletico Madrid
Kipato: Dola 49 milioni.
3. Neymar
Klabu: Paris Saint-Germain
Kipato: Dola 102 milioni.
2. Cristiano
Ronaldo
Klabu: Juventus
Kipato: Dola 126 milioni.
1. Lionel Messi
Klabu: Barcelona
Kipato: Dola 145 milioni.