Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kijo kocha mpya Zanzibar Sand Heroes

UFUKWENI Pict

Muktasari:

  • Ali Shariff Adolf ambaye alikuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Ufukweni Zanzibar (Zanzibar Sand Heroes) na kuichezea timu ya Malindi, alifariki dunia, Ijumaa Juni 6, 2025.

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF), limemteua Kijo Nadir Nyoni kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Zanzibar ya Soka la Ufukweni.

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Juni 27, 2025 na Ofisa Habari wa ZFF, Mohamed Kabwanga, imesema kocha huyo ana diploma C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika(CAF) na alishawahi kupata mafunzo ya ukocha wa Mpira wa Ufukweni kutoka CAF.

Pia Kijo aliwahi kuwa msaidizi wa Timu hiyo iliyoshiriki mashindano ya Beach Soccer kwa mara ya kwanza yaliyofanyika Kenya mwaka 2002.

Kocha Kijo amewahi kufundisha klabu mbalimbali kisiwani Zanzibar ikiwemo Kundemba FC, Uhamiaji FC na Polisi FC.

Kijo amechukua nafasi ya Ali Shariff  Adolf aliyefariki dunia Ijumaa Juni 6, 2025.