Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ibenge awatega mastaa Azam, afichua usajili atakaoufanya

Muktasari:

  • Ibenge amefunguka hayo muda mchache baada ya kusaini mkataba wa kuitumikia klabu hiyo, huku akiweka wazi anaenda kukaa na wachezaji ili waelewe nini anakitaka bila kujali atatumia mfumo gani.

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge amesema atafanya usajili itakapohitajika,  lakini anaamini kikosi kilichopo ni bora kutokana na kumaliza nafasi ya tatu na kupata nafasi ya ushiriki michuano ya kimataifa.

Ibenge amefunguka hayo muda mchache baada ya kusaini mkataba wa kuitumikia klabu hiyo, huku akiweka wazi anaenda kukaa na wachezaji ili waelewe nini anakitaka bila kujali atatumia mfumo gani.

“Kama Azam imemaliza nafasi ya tatu, ni wazi ina timu bora lakini kuna wachezaji wanatoka  hivyo kama kutakuwa na umuhimu tutaingiza wengine, ila  nguvu kubwa ni kuwa na nyota waliofanya makubwa,” amesema Ibenge raia wa DR Congo na kuongeza;

“Siwezi kupambana peke yangu, naomba ushirikiano kutoka kwa wachezaji, viongozi na mashabiki ili niweze kuipambania timu hii iweze kufikia malengo kupambana peke yangu sitaweza.”

Ibenge amesema anapenda kucheza mpira mzuri, lakini anapenda kushinda mechi na mataji, hivyo mashabiki watarajie mambo mazuri kutoka kwake.

Akizungumzia kuhusu ni mfumo gani rafiki atakaoutumia  Ibenge amesema hawezi kuweka wazi, ila anaamini akikaa na wachezaji kwa muda wakimuelewa kila kitu kitakuwa wazi kwenye uwanja wa mechi.