Heh! Coutinho anafanana na Oscar?

Coutinho
MSHAMBULIAJI wa zamani wa Yanga, Ephraim Makoye amestuka baada ya kumwona kiungo mshambuliaji mpya wa Yanga Mbrazil, Andrey Coutinho, akadhani wamemsajili Oscar wa Chelsea.
Makoye amewaambia Simba: “Sasa mmekwisha.”
“Ukimwangalia amefanana kabisa na Oscar kuanzia sura hadi mwili wake ila sijamwona kama anaweza kuwa na kiwango kama cha Oscar ngoja tumwone uwanjani anaonekana ni mchezaji mzuri na mimi namjua kocha maximo hawezi kuleta mtu wa ovyo,”alisema Makoye.
Makoye amesema ameanza kuona mwanga wa mafanikio baada ya kutua kwa kocha Marcio Maximo lakini akaonya asihukumiwe kwa mechi mbili au tatu badala yake apewe nafasi ya miaka miwili ili kuleta mafanikio zaidi.
“Tumwache kwanza Maximo tumpe nafasi ili alete neema kwenye timu yetu ya Yanga amekuja kocha ninayemwamini sana sasa tutatisha pale Jangwani tumpe muda wa kutengeneza kikosi chake hatari ambacho kitakuwa ni tishio kubwa haswa kwa Simba,”alisema Makoye.