Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Guardiola ahofia kufukuzwa Man City

Muktasari:

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amesema ana hofu ya kutimuliwa endapo wataondolewa na Real Madrid katika Ligi ya Mabin gwa Ulaya

London, England. Kocha wa Manchester Citym, Pep Guardiola amesema ana hofu ya kufukuzwa endapo watafungwa na Real Madrid.

Licha ya kuipa Man City ubingwa wa England mara mbili, kocha huyo ana hofu ya kutimuliwa wakifungwa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

“Kama tutashindwa kuifunga Real Madrid, mwenyekiti atakuja au mkuregenzi wa ufundi atasema tunataka ubingwa wa Ulaya, naweza kukufukuza,”alisema Guardiola.

Man City imepoteza matumaini ya kutetea ubingwa mbele ya Liverpool ambayo inaongoza kwa tofauti ya pointi 22 baina yao.

Real Madrid itasafiri kwenda Etihad kuifuata Man City Februari 19 kabla ya kurudiana wiki tatu baadaye nchini Hispania.

“Ndoto yangu ni kutwaa ubingwa wa Ulaya, ingawa wapo wanasema tunacheza kwa kiwango bora na wengine wanasema hapana,”alisema Guardiola.

Kocha huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich, alidai matumaini yake ni kuifunga Real Madrid katika mchezo ujao na kujipanga vyema kwa mechi ya marudiano.