Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Bongo Zozo ala shavu Jingine

Muktasari:

Akizungumza na Mwanaspoti kutoka Iringa, Bongo Zozo alisema amefurahishwa na uteuzi huo uliofanywa na Wanapaluhengo akidai amevutiwa nao zaidi kuliko angepewa wa klabu kubwa nchini.


SIKU chache tangu ateuliwe kuwa, Balozi wa Maliasili na Utalii, shabiki maarufu wa Taifa Stars, Nick Reynolds ‘Bongo Zozo’ amelamba shavu jingine la kuwa balozi katika klabu ya Lipuli FC.

Bongo Zozo jana (Jumatano) akiwa katika ofisi za Lipuli mkoani Iringa, alitangazwa kuwa balozi wa klabu hiyo na kuanza kazi mara moja ya kuhamasisha mashabiki wazidi kuipenda timu hiyo.

Akizungumza na Mwanaspoti kutoka Iringa, Bongo Zozo alisema amefurahishwa na uteuzi huo uliofanywa na Wanapaluhengo akidai amevutiwa nao zaidi kuliko angepewa wa klabu kubwa nchini.

“Nimekuwa nikipenda kushangilia timu ndogo siku zote ndio maana imekuwa rahisi kuwa na mapenzi na Lipuli, nilivyokuja Tanzania nilikaa na kutafuta maisha mkoani Iringa,’’ alisema.

Aliongeza kwa kusema; “Waliponitafuta na kutaka niwe balozi sikuona sababu ya kukataa, nipo tayari kufanya fujo zisizoumiza,” alisema raia huyo wa Uingereza ambaye amekuwa bega kwa bega kuipiga tafu Taifa Stars na kumshangilia Mbwana Samatta ndani ya timu yake ya Aston Villa.