Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ashraf, Zungu kuzichapa Dar es Salaam Jumapili

Muktasari:

Kinondoni ndiko wametokea mabondia, Omari na Said Yazidu, Dullah Mbabe na Francis Miyeyusho ambao walitamba.

Dar es Salaam. Mabondia wa Zanzibar, Ashraf Suleiman na Amour Zungu watapanda ulingoni katika pambano la kuhamasisha ngumi wilaya ya Kinondoni.

Pambano hilo la uzani wa juu litapigwa kwenye ukumbi wa CCM Mwinjuma, Kinondoni likitanguliwa na mengine 10.

Promota wa pambano hilo, Ibrahim Kamwe "Big right" amesema lengo la mapambano hayo ni kurejesha morali ya ngumi Kinondoni.

"Hivi sasa ngumi zinachezwa zaidi Mabibo na Manzese, lakini tunahitaji kurejesha morali hiyo Kinondoni kama ilivyokuwa awali.

Kinondoni ndiko wametokea mabondia, Omari na Said Yazidu, Dullah Mbabe na Francis Miyeyusho ambao walitamba.