Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Andrew afanya kweli michuano ya baiskeli Arusha

Andrew afanya kweli michuano ya baiskeli Arusha

ARUSHA. Mwendesha baiskeli chipukizi kutoka Arusha  Andrew Massawe amefanikiwa kuibuka mshindi katika mashindano ya mchezo huo wa "Burka Mountain bike" yaliyomalizika asubuhi hii mkoani Arusha.

Massawe amefanikiwa kuwa mshindi baada ya kumalizika jumla ya kilomita 50 akitumia saa 1:52:01 na kuwaacha Noel Solomon aliyefika nafasi ya Pili kwa saa 1:53:12 huku Kelvin Didas akimaliza nafasi ya tatu  kwa saa 1:54: 07.

Mashindano hayo ya Burka Mountain bike yamefanyika leo jumapili katika viwanja vya Burka vilivyoko  eneo la Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.

Akizungumzia ushindi wake Massawe alisema kuwa ni Mara ya kwanza yeye kushinda mashindano hayo aliyoshiriki Mara mbili mfululizo.

"Kila nikija kushiriki nakoa hata nafasi tano za juu, lakini tangu huu mwezi umeanza nilijiwekea malengo ya kutaka kushinda na nimefanikiwa sitaachia nafasi hii" alisema Massawe