Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

29 wa kigeni wakoleza utamu BDL

BDL Pict

Muktasari:

  • Idadi ya nyota hao imekuwa ikiongezeka na wamesajiliwa katika timu mbalimbali zinazoshiriki ligi hiyo na waliopo hadi sasa ni 29.

USHINDANI na uwepo wa nyota wa kigeni katika Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL), umeifanya izidi kuimarika na kuwa moja ya zinazoongoza kwa ubora Ukanda wa Afrika Mashariki.

Idadi ya nyota hao imekuwa ikiongezeka na wamesajiliwa katika timu mbalimbali zinazoshiriki ligi hiyo na waliopo hadi sasa ni 29.

Wachezaji hao wanatoka katika timu za Dar City, Srelio, DB Oratory, Savio, Pazi na upande wanawake ni DB Oratory, DB Lioness na Pazi Queens

Dar City ilisajiri wachezaji wanne ambao ni Victor Mwoka (Kenya), Jamel Marbuary (Marekani) na Clinton Best (Nigeria).

Mchezaji Larry Mve (Gabon), Dan Kola (Congo), Junior Lousisi (Gabon) na Kabangu Mrc (Congo), wamesajiliwa na timu ya Srelio

DB Oratory imewasajiii   Thitenkas Chad (Congo), Kakumbuka Henock (Congo), Hassan Kabanda (Uganda) na Oswald Bera (Congo).

Savio  imewasajili   Ntibonela Bukeng   (Congo), Chelord Kabantu (Congo), Ludovick Zentang (Comoro),  huku  Kurasini Heat ikiwa na  Zadock  Emmanuel (Kenya) na Tshiband Anachet (Congo).

Kwa upande wa  timu ya Pazi ina Robert Tasire (Uganda), Soro Geofrey (Uganda), Yang Ugweno (Kenya) Trevor Petar (Kenya), Sam Agutu (Kenya

Kwa upande wanawake,  Pazi Queens imewasajili  Marline Salumu (Congo), Veronica  Aluvel (Sudan) na Chantal Dunia (Congo).

DB Lioness imemsajili Taudencia Katumbi (Kenya) Lawender Obinda (Kenya), Sokouudjou Michele (Comoro), Christaian Akinyi (Kenya) na Cynthia Wafula (Kenya).

Timu ambazo hazina  wachezai wa kigeni upande wanaume ni  KIUT, Vijana ‘City Bulls’, Mgulani JKT,  ABC na JKT na kwa wanawake ni Ukonga Queens, Twalipo Queens, Vijana Queens.