Klabu ya Simba imeibuka na ushindi wa mabao 8-0 dhidi ya Eagle katika michezo ya raundi ya pili kwenye Kombe la Shirikisho Azam (ASFC) mchezo uliochezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Vilevile Ihefu imeinyeshea mvua ya mabao 9-0 timu ya Mtama Boys mchezo uliochezwa uwanja wa Highland Estate, Mbeya.
Kocha mpya wa Ruvu Shooting Mbwana Makata amenza kibarua chake vyema kwenye Kombe la ASFC akiisaidia timu yake kuifunga Ndanda FC mabao 4-1.