UCHAMBUZI: Thierry Henry katika shimo jingine la Diego Maradona

Aliwahi kujisemea mtu aliyeitwa Mae West, You only live once, and if you do right, once is enough. Nadhani alikuwa anamaanisha hivi kwa Kiswahili sahihi. Unaishi mara moja tu, na kama unafanya kila kitu kwa usahihi basi, mara moja inatosha’

Mae, mwanamitindo, muigizaji na mwanamuziki mahiri wa enzi zake ambaye alifia Hollywood mwaka 1980 huenda alikuwa sahihi sana. Wakati mwingine unageuza mtazamo na kuacha kuyatazama maisha kwa ujumla. Unaitazama tu kazi fulani kwa ujumla.

Unajikuta uliifanya kazi hiyo vyema. Ukaibeba vyema. Ikakupa umaarufu. Inatosha. Ukihamia kwingine unaharibu. Sio wote wanaoharibu. Lakini sio wote wanaofanikiwa. Wengi hufeli. Nahisi mmoja kati ya hao wengi ni Thierry Daniel Henry.

Fuatana na Edo Kumwembe kupata uchambuzi huu kwa kubonyeza:https://fupi.co.tz/jPbWh04