Sakho, Mayele mwendo wa pesa tu! Banda, Makambo nao ndani

Muktasari:

HAKUNA siri, madini ni moja ya rasilimali zinazoliingiza taifa mapato makubwa kutokana na thamani yao. Lakini kama hujui hata kwenye soka kwa sasa kuna ‘madini’ mengine ambayo yamekuwa yakiliingiza soka mkwanja wa maana. Ni nyota wa kigeni wanaosajiliwa na klabu mbalimbali nchini kila msimu.

HAKUNA siri, madini ni moja ya rasilimali zinazoliingiza taifa mapato makubwa kutokana na thamani yao. Lakini kama hujui hata kwenye soka kwa sasa kuna ‘madini’ mengine ambayo yamekuwa yakiliingiza soka mkwanja wa maana. Ni nyota wa kigeni wanaosajiliwa na klabu mbalimbali nchini kila msimu. Klabu zimekuwa zikisajili nyota wa kigeni kutoka nje ya nchi ambao wamekuwa wakilitunisha mfuko wa soka kwa namna fedha zinazotozwa kwa kuwepo kwao haopa nchini, kiasi hata zile kelele za wadau kwamba ongezeko la wageni katika Ligi Kuu Bara ni msala, hakuna anayezisikiliza.

Wingi wa maproo hao umekuwa na faida nyuma yake hata nje ya soka.

Kwa taarifa ambazo Mwanaspoti limezinyaka kwa msimu huu kuna wachezaji wa kigeni 77 na kila mmoja hulipa Sh 4 milioni TFF kwa mwaka ambapo ni sawa na Sh 333,333 kwa mwezi na kwa jumla yao inaonyesha TFF huvuna kiasi cha Sh 308 milioni kwa mwaka.

Upande wa Uhamiaji mchezaji hulipa dola 2050 sawa na wastani wa Sh 4.7 milioni ili kupata kibali cha kuishi hii haijalishi mkataba wake na timu ni wa muda gani kwani hulipa mara moja kulingana na mkataba wake wa kazi. Hivyo serikali huingiza Sh 360 milioni kwa mwaka.

Kwa upande wa Wizara ya Kazi, kila mchezaji hulipa dola 1000 wastani wa Sh 2.3 milioni hivyo kwa wachezaji 77 huingiza kiasi cha zaidi ya Sh 154 milioni.

Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wenyewe huchukuwa dola 500 wastani wa Sh 1 milioni kwa kila mchezo hivyo kwa mwaka kwa wachezaji 77 huingiza Sh 77 milioni.

Dirisha la usajili la wachezaji lilifungwa usiku wa Agosti 31 na jumla ya mataifa 16 yapo kwenye Ligi Kuu pamoja na Championship League (zamani Ligi Daraja la Kwanza).

Kwa upande wa soka la wanaume Taifa la Congo DRC ndio linaongoza kuwa na wachezaji wengi (16) huku Yanga pekee ikiwa na Wakongo saba, Uganda wachezaji (9), Burundi (8), Ghana na Kenya (7).

Zambia na Zimbabwe (5) Cameroon (4), Malawi (3), Nigeri, Bukina Faso, Rwanda na Mali (2), Senegal, Ivory Coast, Msumbiji wakiwa na mchezaji mmoja na kufanya jumla ya wageni 77.

Wachezaji hao wanatoka kwenye timu tisa za Ligi Kuu na timu nne za FDL huku Yanga na Simba zikionekana kuwa na wachezaji wengi zaidi (12) na Azam akiwa na wageni 10 na kule FDL, DTB ikisajili wageni saba.

Kwa upande wa Ligi Kuu ya Wanawake ina jumla ya wachezaji 33 na Kenya inaongoza kuwa na idadi kubwa ya wachezaji hapa Tanzania wakiwa na wachezaji 19.

Nayo TSC Queens ikiwa na wachezaji saba wote raia wa Kenya huku The Tiger Queens ikiwa na wachezaji wengi zaidi kuliko timu yoyote (8), hivyo kufanya jumla ya wachezaji wa kigeni 110.

Kwa maana hiyo TFF inaingiza kwa mwaka mmoja Sh 308,000,000 milioni kwa upande wa Ligi Kuu Bara na FDL kwa upande wa Ligi Kuu ya Wanawake wapo 33 ina maana TFF inaingiza Sh 132,000,000 milioni kwa mwaka na kufanya kwa mwaka kukusanya Sh 440,000,000 milioni.

Mwanaspoti linakuletea kila timu na idadi ya wachezaji wageni waliokuwa kwenye timu hizo.

DTB FC -7

Amissi Tambwe - Burundi

Danny Phiri - Zimbabwe

Emmanuel Ngama - Burundi

Hemedy Murutabose - Burundi

Nicholas Gyan- Ghana

Owen Chaima - Malawi

Tafadzwa Kutinyu - Zimbabwe


GWAMBINA FC -4

Kone Moustapha - DR Congo

Ndongo Michel - Cameroon

Olivier Kabangu - DR Congo

Wandaman Kabongo -Congo


KITAYOSA FC -2

Katende Elie - DR Congo

Tshama Nsumbu- DR Congo


AFRICAN LYON -2

Apheal Femi Aloba - Nigeria

Solomon Mutapili -Zimbabwe


SIMBA -12

Baka Inonga-DR Congo

Banda Peter- Malawi

Bernard Morrison-Ghana

Bwalya Rally- Zambia

Duncan Nyoni- Malawi

Kagere Medie-Rwanda

Kanoute Sadio- Mali

Chriss Mugalu- DR Congo

Onyango Joash - Kenya

Pape Sakho - Senegal

Pascal Wawa - Ivory Coast

Taddeo Lwanga - Uganda


YANGA -12

Bangala Yannick - DR Congo

Djigui Diarra - Mali

Djuma Shabani - DR Congo

Fiston Mayele - DR Congo

Heritier Makambo -DR Congo

Jimmy Ukonde - Msumbiji

Khalid Aucho - Uganda

Moloko Jesus - DR Congo

Mukoko Tomombe - DR Congo

Saidi Ntibazonkiza - Burundi

Yacouba Songne- Burkina Faso


AZAM FC -10

Bruce Kangwa - Zimbabwe

Charles Zulu - Zambia

Daniel Amoah -Ghana

Kenneth Muguna - Kenya

Mathias Kigonya-Uganda

Nico Wadada - Uganda

Paul Katema -Zambia

Prince Dube -Zimbabwe

Rodgers Kola

- Zambia

Yvan Mballa - Cameroon


BIASHARA UNITED -7

Ambrose Awio - Uganda

Baron Oketch - Kenya

Christian Zigah - Ghana

James Ssetuba - Uganda

Metthew Odongo-Uganda

Opare Collins - Ghana

Shaphan Siwa- Kenya


NAMUNGO FC -6

Bigirimana Blaise - Burundi

David Molinga- Dr Congo

Eric Kwizera - Burundi

Jonathan Nahimana - Burundi

Obrey Chirwa - Zambia

Stephen Sey - Ghana


COASTAL UNION -5

Joseph Zziwa - Uganda

Ngamchiya Amza - Cameroon

Pasco Kitenge - DR Congo

Sosthenes Idah - Kenya

Victor Akpan - Nigeria

KAGERA SUGAR -5

Nouridine Balora -Burkina Faso

Ppolinaire Tientcheu- Cameroon

Ackson Harodi-Uganda

Stephen Duah- Ghana

Timothy Omwenga- Kenya


KMC FC -3

Emmanuel Mvuyekure- Burundi

Faruk Shikhalo- Kenya

Jean Mugiraneza -Rwanda


MTIBWA SUGAR -2

Boban Zirintusa -Uganda

Nzigamasabo Styve- Burundi


LIGI KUU YA WANAWAKE

ALLIANCE GIRLS-3

Anita Agunda-Kenya

Eliver Mungo-Kenya

Florida Omusanga-Kenya


BAOBAB QEENS-1

Jeanne Pauline-Rwanda

FOUNTAIN GATE PRINCESS FC-4

Carolyne Rufa-Kenya

Faith Machora-Kenya

Niyonkuru Sandrine-Burundi

Pauline Kathuruh-Kenya


RUVUMA QUEENS-3

Fanis Kwamboka-Kenya

Nakasumba Fatumah-Uganda

Rachele Gakima-Burundi


SIMBA QEENS-4

Asha Djafari-Burundi

Danai Bhobho-Zimbabwe

Joelle Bukuru-Burundi

Musolo Mawete-DR Congo


TIGER QUEENS-8

Alice Kalimba-Rwanda

Diana Koske-Kenya

Drailer Sati-Kenya

Elizabeth Katungwa-Kenya

Linda Kihara-Kenya

Natasha Witika-Zambia

Samantha Okeya-Kenya

Zakia Umubyeyi-Rwanda


TSC QUEEN -7

Cynthia Matekwa-Kenya

Fridhaus Mwakaga-Kenya

Meali Bakari-Kenya

Micky Emma-Kenya

Nanzugu Chilo-Kenya

Vereneta Mkoa-Kenya

Zaithuni Ali-Kenya


YANGA PRINCESS -3

Aniella Uwimana-Burundi

Daniela Kanyanya-DR Congo

Olga Kalamba-DR Congo