Mwana FA, Nikki wa Pili wateka jukwaa mbele ya Rais Samia

Mwana FA, Nikki wa Pili wateka jukwaa mbele ya Rais Samia

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Nickson Simon maarufu Nikki wa Pili na Mbunge wa Muheza (CCM), Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA wameungana na Sugu na wasanii wengine kuteka jukwaa walipoimba pamoja mbele ya Rais Samia kwenye tamasha hilo.

Huku akitabasamu, mshereheshaji alimuuliza Rais Samia amewaonaje vijana wake ambao ni viongozi kwenye Serikali yake wakipafomu?

Hata hivyo Rais Samia kwa muda huo hakujibu chote zaidi ya kutabasamu.

Baadaye wakati akitoa hutuba yake, Rais Samia aliweka wazi kuwa kuna kipindi alikuwa mtazamo kuwa mziki wa HipHop ni uhuni huku akieleza kuwa mtazamo huo umebadilika.

"Hata mimi nilipokuwa nikiwaona wanafoka foka niliona uhuni wakati ule, lakini kumbe sio kweli, muziki umeleta heshima," amesema.

Kuhusu wateule wake na wabunge ambao wako kwenye tasnia hiyo ya muziki, Rais Samia amebainisha kuwa hawezi kuwaingilia kwa kuwa wanaweza kujipanga katika kutimiza majukumu yao.

"Hapa wasanii wameimba sijasikia maneno ya kukera, nimeona wabunge na wakuu wa wilaya wakiimba, nikajiuliza wanafanya kazi saa ngapi, lakini wanajua wanavyojigawa, simvunji moyo, nimebariki aendelee tu," amesema Rais Samia.