Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Dude amtolea uvivu Q-Chillah

Dude

Muktasari:

“Napenda kumwambia mdogo wangu Q-Chillah huku siyo kama katika muziki, huku tunavaa kulinga na uhusika, siyo kuvaa tu ilimradi umevaa tu, maskini hawezi kuvaa suti, au mchungaji kuvaa pensi au kuonekana tofauti na hadithi inavyosema.

MWONGOZAJI na mwigizaji mkongwe katika tasnia ya filamu Swahilihood, Kulwa Kikumba ‘Dude’ amemtolea uvivu msanii wa muziki wa kizazi kipya na mwigizaji wa filamu, Shabani Katwila ‘Q-Chillah’ kwa kumwambia kuwa katika filamu hakuna ubishoo zaidi ya uhalisia na uhusika kwa filamu husika.

“Napenda kumwambia mdogo wangu Q-Chillah huku siyo kama katika muziki, huku tunavaa kulinga na uhusika, siyo kuvaa tu ilimradi umevaa tu, maskini hawezi kuvaa suti, au mchungaji kuvaa pensi au kuonekana tofauti na hadithi inavyosema.

“Namkumbusha Q-Chillah huku kugumu kuliko kwenye muziki anakotaka na tunavaa kulinga na uhusika hakuna ubishoo,” alisema.

Dude alisema hayo kufuatia kauli ya Q- Chillah kuwa wasanii wengi wa filamu hawajipangi katika mavazi, wakati yeye anapoingia katika filamu yoyote anajipanga na kununua nguo za kutosha hadi kutumia milioni kwa ajili ya filamu anayoigiza.