Ugarte kajiweka kwa X wa Mbappe

Muktasari:
- Cunha,ambaye alisajiliwa kwa Pauni 62.5 milioni kutoka Wolves alikuwa mchezaji wa kwanza kuripoti kambini kwenye viwanja hivyo vya mazoezi vya Man United, akiwasili kabla ya saa 2 asubuhi.
MANCHESTER, ENGLAND: STAA mpya wa Manchester United, Matheus Cunha amedhamiria kumshawishi kocha Ruben Amorim katika siku yake ya kwanza ya ‘pre-season’ huko Carrington, Jumatatu.
Cunha,ambaye alisajiliwa kwa Pauni 62.5 milioni kutoka Wolves alikuwa mchezaji wa kwanza kuripoti kambini kwenye viwanja hivyo vya mazoezi vya Man United, akiwasili kabla ya saa 2 asubuhi.
Staa huyo wa Kibrazili, 26, aliungana na mchezaji mwenzake mpya Diego Leon, sambamba na mastaa wengine, Amad, Mason Mount, Noussair Mazraoui, Ayden Heaven, Joshua Zirkzee, Toby Collyer, Matthijs De Ligt na Kobbie Mainoo. Kwa ujumla, wachezaji 15 walikuwapo siku ya kwanza mazoezini.
Wachezaji wengine kwenye kikosi hicho watawasili wiki hii, isipokuwa wachezaji watano – Marcus Rashford, Alejandro Garnacho, Antony, Tyrell Malacia na Jadon Sancho – ambao wameambiwa na klabu hiyo watafute timu za kwenda.
Kinachoelezwa ni kwamba wachezaji hao watano wataruhusiwa kufanya mazoezi kwenye viwanja hivyo mara tu kocha Amorim na kikosi chake watakapoondoka kwenda kwenye ziara ya mechi za pre-season huko Marekani.
Rashford, ambaye nusu ya msimu uliopita alikuwa kwa mkopo Aston Villa, alipoteza jezi Namba 10 iliyokabidhiwa kwa Cunha, hivyo anapambana kuachana na timu hiyo. Anataka kwenda kujaribu bahati yake nje ya nchi, huku Barcelona ikitajwa kuwa huenda ikawa sehemu atakayoenda.
Kocha wa Man United, Amorim atahitaji kukiweka kikosi chake kwenye kiwango bora kabisa ili isiwe kama msimu uliopita, wakati timu hiyo ilipomaliza nafasi ya 15 kwenye msimamo wa Ligi Kuu England. Man United ilikuwa na wakati mgumu baada ya kuchapwa kwenye fainali ya Europa League na wapinzani wao wa Ligi Kuu England, Tottenham Hotspur huko Bilbao, Hispania.
Man United iliwapa ruhusa nahodha wao Bruno Fernandes na beki Diogo Dalot siku za ziada kwa ajili ya kuomboleza msiba wa mchezaji mwenzao wa kimataifa wa Ureno, Diogo Jota, aliyefariki dunia kwenye ajali ya gari huko Hispania asubuhi ya Alhamisi na kuzikwa Jumamosi.