Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Uamuzi wa VAR wamkera Ferdinand, 'akomalia' bao la Konate

Muktasari:

  • Maxime anachukua nafasi ya Malale Hamsini ambaye licha ya kuanza msimu vizuri, lakini ghafla mambo yalibadilika na pande hizo mbili kukubaliana kuachana.

Rio Ferdinand amezua hisia mtandaoni baada ya uamuzi wa VAR kufuta bao la Ibrahima Konate katika mechi ya Liverpool dhidi ya Inter Milan ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Konate alifunga kwa kichwa kipindi cha kwanza, lakini bao lilifutwa baada ya VAR kubaini Virgil van Dijk aligusa mpira kwa mkono kabla ya Konate kuufikisha wavuni.

Mwamuzi Felix Zwayer alipelekwa kwenye ‘Skrini’ kufanya uamuzi wa mwisho, baada ya ukaguzi wa VAR wa dakika tano. Ferdinand aliandika kwenye X: “Uamuzi mkali sana. Ilikuwa nafasi muhimu na inayohitajika kwa Konate! Pia kwa nini waamuzi hawapelekwi kwenye ‘Skrini’ mapema ili kuharakisha mechi?”

Mashabiki wa klabu mbalimbali walitoa maoni yao mtandaoni, wakiisifu Liverpool lakini pia wakionyesha kushangazwa na uamuzi huo. Mmoja alisema: “Sina uhusiano na Liverpool, lakini kufuta bao hilo la mkono ni kashfa.”

Kulingana na kanuni za IFAB zinazotumika na UEFA, bao la mkono hutolewa ikiwa mchezaji ‘atausogeza mkono kuelekea kwenye mpira’ au ‘mkono unafanya mwili kuwa mkubwa isivyo kawaida.’

Uamuzi huo umepandisha mjadala mtandaoni kuhusu utumiaji wa VAR na jinsi inavyoweza kuathiri matokeo ya mechi kubwa.

Sakata hili linaonesha jinsi teknolojia katika soka la kisasa inavyoweza kuleta hisia mchanganyiko, huku wapenzi wa Liverpool wakihisi Konate alikosa haki kwenye tukio hilo muhimu