Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

TRIONDA: Mpira wa ‘AI’ Kombe la Dunia 2026

MPIRA Pict

Muktasari:

  • Mpira huo unaoitwa Adidas Trionda unauzwa takriban Dola 160 ukiwa umetengenezwa kwa namna ambayo haisaidii tu wachezaji, bali pia waamuzi kwani ndani yake kuna teknolojia inayosaidia katika uamuzi ya ‘offside’.

NYON, SWITZERLAND: SHIRIKISHO la Kandanda Duniani (Fifa) limezindua mpira utakaotumika katika Kombe la Dunia 2026 ambao una maboresho kibao ya kiteknolojia ikiwemo  akili unde (AI).

Mpira huo unaoitwa Adidas Trionda unauzwa takriban Dola 160 ukiwa umetengenezwa kwa namna ambayo haisaidii tu wachezaji, bali pia waamuzi kwani ndani yake kuna teknolojia inayosaidia katika uamuzi ya ‘offside’.

Rangi zake ni nyeupe, nyekundu, bluu na kijani zikibeba alama za mataifa yatakayokuwa wenyeji wa mashindano ambayo ni Marekani, Canada na Mexico na kwa mwonekano unafanana kidogo na ule mpira wa Brazuca uliotumika katika Kombe la Dunia 2014 kule Brazil.

MPI 03

Mpira huo una nyota ya bluu ambayo inawakilisha Marekani, jani jekundu la ua la maple linalo wakilisha Canada na pia kuna tai wa kijani kama alama ya Mexico

Sam Handy, makamu wa rais wa Adidas anayeshulika na ubunifu amesema: “Huu ndio mpira wa Kombe la Dunia ulio na mwonekano wa kuvutia zaidi tuliowahi kutengeneza. Tumeuandaa kwa kuzingatia kwamba utatumika katika mashindano makubwa zaidi duniani na ubora wake hautakufanya uishie kuutazama tu, bali utatamani kuucheza, kuushika na kuutazama.”

Ndani ya mpira huo kuna ‘chip’ maalumu ambayo inatuma taarifa moja kwa moja kwenye mfumo wa VAR.

MPI 01

Vilevile mpira huo umefungwa kifaa maalumu ambacho kinakusanya taarifa ikiwa ulishikwa mkononi na ikiwa mchezaji aliyekuwa nao aliotoea au la.

Katika matangazo ya uzinduzi, nyota wa Real Madrid, Jude Bellingham Lionel Messi wa Inter Miami na Lamine Yamal wa Barcelona walionekana wakifurahia kuuchezea.

Mojawapo wa picha ilimuonyesha Lamine Yamal akiwa ameshika mpira mkubwa mno na baadaye baadhi ya mashabiki wakaanza kusema atawezaje kuutumia kucheza, lakini Fifa ikatoa ufafanuzi kwamba huo ulikuwa ni mfano. 

MPI 02

Hata hivyo, mipira ya mashindano ya hivi karibuni ukiondoa ule wa Kombe la Dunia 2014, mara nyingi imekuwa ikikosolewa na wachezaji kuwa na uelekeo tofauti pale inapopigwa kwenda juu.

“Mpira huu umeundwa kwa ajili ya tukio kubwa zaidi la michezo duniani. Huu ni mpira wa kwanza wa aina yake ukiwa na teknolojia ya maalumu  na umeunganishwa na mfumo wa AI  ili kutoa data na taarifa za papo kwa papo zitakazosaidia kila kitu kuanzia uamuzi wa waamuzi hadi uchambuzi wa matukio,” imesema taarifa ya Adidas.