Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Staa avunjika mifupa ya shingo, hatarini kupooza

ASAMOAH Pict

Muktasari:

  • Nyota huyo mwenye umri wa miaka, 31, aliyekuwa akiichezea klabu yake  Guangxi Pingguo katika mechi dhidi ya Chongqing Tonglianglong katika ligi daraja lapili nchini China alipata ajali mbaya baada ya kujigonga katika bango na kuvunjika shingo.

BEIJING, CHINA: NYOTA wa kimataifa wa Togo,  Samuel Asamoah  yupo katika hatari kubwa ya kupooza mwili mzima  baada ya kujigongana vibaya katika bango la matangazo Uwanjani.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka, 31, aliyekuwa akiichezea klabu yake  Guangxi Pingguo katika mechi dhidi ya Chongqing Tonglianglong katika ligi daraja lapili nchini China alipata ajali mbaya baada ya kujigonga katika bango na kuvunjika shingo.

Video iliyorekodiwa wakati wa mechi hiyo, iliyochezwa Jumapili iliyopita, ilionyesha Asamoah akigombania  mpira na kiungo wa  timu pinzani, Zhang Zhixiong na katika harakati hizo, Asamoah alionekana akijigonga kwa  kichwa kwenye bango lililoko kando ya uwanja kisha akadondoka chini  kabla ya madaktari kwenda kumtibu.

ASA 01

Baada ya tukio hilo, siku moja baadae, klabu yake ilitoa taarifa ya kushtua ikisema staa huyo  yupo katika hatari kubwa ya kupooza mwili mzima  baada ya  mifupa mingi shingoni mwake kuvunjika na kukata mishipa ya neva.

Klabu hiyo ilithibitisha kuwa Asamoah alifanyiwa  upasuaji na atakosa mechi zote zilizobaki msimu huu, na kuongeza kuwa , anaweza asionekane tena kiwanjani.

"Guangxi Pingguo FC inashukuru kwa dhati mashabiki wote na watu wengine  kwa kuwa na wasiwasi na kuonyesha nia ya kutaka kutoa msaada kwa  Samuel Asamoah. Maendeleo ya hali yake  yatatangazwa siku zijazo baada ya vipimo zaidi."

Asamoah, ambaye ameichezea Togo katika mechi sita za kimataifa, alitumia sehemu kubwa ya maisha yake ya soka  kucheza Ubelgiji kabla ya kuhamia Romania mwaka 2021, kisha kutua China mwaka 2024 kujiunga na Qingdao Red Lions kwa msimu mmoja kabla ya kujiunga na klabu yake ya sasa.

ASA 02

Tukio hili linafananishwa na lile la nyota wa zamani wa akademi ya Arsenal, Billy Vigar ambaye alifariki mwezi uliopita baada ya kukaa kwenye koma kwa siku 10 kutokana na jeraha kubwa la ubongo.

Vigar, 21, anadaiwa kuwa alipata jeraha hilo baada ya kichwa chake kugonha  ukuta wa zege kando ya uwanja wakati akiicheza  Chichester City inayoshiriki ligi ya madaraja ya chini England.