Mlemavu wa mkono atamba table tenisi

MCHEZAJI Paralimpiki katika mchezo wa table tenisi, Natalia Partyka amefuzu kucheza hatua ya 32 kwa wachezaji moja moja kwa wanawake katika Olimpiki. Mchezaji huyo mwenye miaka 23, wa Poland, aliyezaliwa akiwa hana mkono moja alimshinda Mie Skov wa Denmark kwa 4-3. Partyka ni moja kati ya wanamichezo wawili wenye ulemavu wanaoshiriki Olimpiki na Paralimpiki mwingine ni mkimbiaji wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius. Partyka sasa atacheza na Jie Li wa Uholanzi katika mchezo wa raundi ya tatu.