Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mechi za nyumbani Spurs inaomba dua zenu jamani!

RATIBA Pict

Muktasari:

  • Unajua kwa nini? Spurs imekuwa na kiwango kibaya sana ikiwa nyumbani msimu huu na si kwa viwango vya Ligi Kuu England pekee.

LONDON, ENGLAND: MCHEZA kwao hutuzwa. Lakini, wahenga wa Tottenham Hotspur wanaangaliana usoni huu ya msemo huo wa kihenga.

Unajua kwa nini? Spurs imekuwa na kiwango kibaya sana ikiwa nyumbani msimu huu na si kwa viwango vya Ligi Kuu England pekee.

Timu hiyo imekuwa nyepesi zaidi kwa wapinzani wao inapocheza kwenye uwanja wake wa nyumbani, ambao umejengwa kisasa kabisa.

Spurs ilipoteza tena nyumbani Alhamisi usiku, kwa namna iliyo ya kawaida kabisa kwa timu hiyo inapocheza kwenye uwanja wake msimu huu.

Mchezo ulianza vizuri, huku kikosi cha Igor Tudor kikionekana kuwa na dakika mbili bora zaidi za msimu wao katika kipindi cha kwanza dhidi ya Crystal Palace. Waliepuka kuruhusu bao la kwanza pale Ismaïla Sarr aliponaswa kwenye mtego wa kuotea, kabla ya Dominic Solanke kuipatia Spurs bao la kuongoza.

Lakini, dakika tatu baadaye, mambo yalibadilika vibaya kwa Spurs. Nahodha wao na mchezaji muhimu zaidi, Micky van de Ven, alitolewa kwa kadi nyekundu, jambo lililosababisha kuporomoka kwa timu hiyo. Spurs wakitoka kuongoza dakika ya 38 hadi kuwa nyuma kwa mabao 3–1 huku pia wakiwa pungufu ya mchezaji mmoja kufikia mapumziko ya kipindi cha kwanza.

Kwa baadhi ya mashabiki wa Spurs, hilo lilitosha kuwafanya kuondoka uwanjani mapema. Na kwa kuzingatia kiwango kibaya sana walichokiona katika Uwanja wa Tottenham Hotspur msimu huu, ni nani angewalaumu?

RATI 01

Ikiwa jambo lisilofikirika litatokea na Spurs ikashuka daraja, rekodi ya mbaya ikiwa nyumbani itakuwa moja ya sababu kuu pamoja na kushindwa kwao kushinda mechi popote walipo katika mwaka wa 2026.

Spurs imekusanya pointi 10 tu katika mechi 15 ilizocheza nyumbani msimu huu, ikipoteza mechi tisa kati ya hizo. Ni tofauti ya mabao pekee inayowazuia kuwa na rekodi mbaya zaidi katika Ligi Kuu England.

Katika klabu zote 92 za EFL Championship, EFL League One na EFL League Two, ni Sheffield Wednesday pekee iliokusanya pointi chache zaidi nyumbani kuizidi Spurs. Na klabu hiyo ya Owls ilionekana tayari iko hatarini kushuka daraja kutoka Championship hata kabla msimu haujaanza, wakati Thomas Frank bado alikuwa na matumaini makubwa kuhusu msimu ujao.

RATI 02

Barani Ulaya, katika ligi tano kubwa, ni klabu za Hellas Verona, Pisa SC, FC Metz, FC Nantes na VfL Wolfsburg pekee ambazo zimepata pointi chache zaidi nyumbani.

Hata hivyo, zote zimecheza mechi chache za nyumbani kuliko Spurs, na ni Pisa pekee inaoweza kulingana na Spurs kwa kupoteza mechi tisa nyumbani. Spurs bado ina mechi nne za nyumbani zilizobaki katika Ligi Kuu England; mechi muhimu dhidi ya Nottingham Forest, Leeds United, Brighton na Everton.

RATI 03

Forest, Brighton na Everton zote zimekusanya pointi nyingi zaidi zikiwa ugenini kuliko Spurs walizopata nyumbani, wakati rekodi ya Leeds ugenini kwa sasa inalingana na rekodi ya Spurs inapocheza nyumbani. Takwimu hizo si habari njema kabisa kwa Spurs na rekodi yake katika mechi za nyumbani ilizocheza msimu huu kwenye Ligi Kuu England.

MSIMAMO WA MECHI ZA NYUMBANI LIGI KUU ENGLAND

                                P        W       D        L        GF      GA      GD      PTS

1.Man City            15       11        3        1         36      11        +25    36

2.Arsenal               14       11        2        1         33      9        +24    35

3.Man United        14       9        3        2        27      16       +11      30

4.Aston Villa          15       9        2        4        21       15       +6      29

5.Liverpool             14       8        3        3        26      16       +10    27

6.Sunderland         14       7        5        2        22      13       +9      26

7.Fulham                15       8        2        5        24      18       +6      26

8.Newcastle           15       8        2        5        28      24      +4      26

9.Brentford            14       7        4        3        24      15       +9      25

10.Bournemouth   15       6        7        2        21       15       +6      25

11.Brighton            15       6        6        3        22      16       +6      24

12.Chelsea             14       6        5        3        23      16       +7      23

13.Leeds                 15       6        4        5        22      20      +2      22

14.Everton               15       5        4        6        18       19       -1       19

15.Crystal Palace   14       3        6        5        14       18       -4      15

16.Nottm Forest     14       3        4        7        13       19       -6      13

17.West Ham           14       3        3        8        17       27      -10     12

18.Wolves                16       3        3        10      17       31       -14     12

19.Tottenham         15       2        4        9        18       25      -7      10

20.Burnley                14       2        4        8        15       23      -8      10