Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Madrid, PSG zasubiri mchujo UEFA

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

  • Timu zilizofuzu moja kwa moja 16 Bora ni zilizomaliza ndani ya nane bora katika hatua ya ligi ambazo ni Arsenal, Bayern Munich, Liverpool, Tottenham, Barcelona, Chelsea, Sporting Lisbon na Manchester City. Hata hivyo, bado haijajulikana zitapangwa dhidi ya timu zipi katika hatua ya mtoano.

JANA usiku, zimepigwa mechi 18 za Ligi ya Mabingwa Ulaya kuhitimisha mfumo wa ligi ambapo sasa zimefahamika timu nane zilizofuzu moja kwa moja hatua ya 16 Bora, huku zingine 16 zikisubiri kucheza mtoano ili zifuzu zikiwamo Real Madrid, PSG na Inter Milan.

Timu zilizofuzu moja kwa moja 16 Bora ni zilizomaliza ndani ya nane bora katika hatua ya ligi ambazo ni Arsenal, Bayern Munich, Liverpool, Tottenham, Barcelona, Chelsea, Sporting Lisbon na Manchester City. Hata hivyo, bado haijajulikana zitapangwa dhidi ya timu zipi katika hatua ya mtoano.

Timu zilizomaliza nafasi ya 9 hadi 24 kwenye hatua ya ligi, zitachuana katika mechi za nyumbani na ugenini ili kupata washindi nane watakaofuzu kwenda hatua ya 16 bora.

Kulingana na nafasi walizomaliza kwenye ligi, timu ya 9 na 10 zitacheza dhidi ya moja kati ya timu za 23 au 24. Timu ya 11 na 12 zitakutana na moja kati ya timu za 21 au 22. Mfumo huu unaendelea kwa mpangilio huo hadi kukamilisha mchujo huo.

Kwa mfano, Real Madrid (nafasi ya 9) na Inter Milan (nafasi ya 10) zitakutana na moja kati ya Bodo/Glimt au Benfica (nafasi ya 23 na 24). Ni droo ya mtoano itakayoamua nani atacheza na nani hasa.

Ni muhimu kutambua kuwa, timu kutoka nchi moja zinaweza kukutana katika hatua hii, huku pia timu zilizokutana tayari kwenye hatua ya ligi pia zinaweza kupangwa tena.

Droo ya mtoano itafanyika katika makao makuu ya UEFA nchini Uswisi, kesho Ijumaa, Januari 30, 2026 kuanzia saa 8:00 mchana kwa saa za Afrika Mashariki.

Mechi za mtoano zitachezwa katika wiki za katikati ya Februari 2026 ambapo mechi za mkondo wa kwanza ni Februari 17 na 18 na marudiano Februari 24 na 25.

Baada ya kukamilika kwa mechi hizo za mtoano, droo ya hatua ya 16 bora, robo fainali na nusu fainali itafanyika Februari 27, 2026.


ZITAKAZOCHEZA MTOANO

Nafasi ya 9: Real Madrid

Nafasi ya 10: Inter Milan

Nafasi ya 11: PSG

Nafasi ya 12: Newcastle

Nafasi ya 13: Juventus

Nafasi ya 14: Atletico Madrid

Nafasi ya 15: Atalanta

Nafasi ya 16: Bayer Leverkusen

Nafasi ya 17: Borussia Dortmund

Nafasi ya 18: Olympiakos

Nafasi ya 19: Club Brugge

Nafasi ya 20: Galatasaray

Nafasi ya 21: Monaco

Nafasi ya 22: Qarabag

Nafasi ya 23: Bodo/Glimt

Nafasi ya 24: Benfica



MATOKEO MECHI ZA JANA

Ajax 1–2 Olympiacos

Arsenal 3–2 Kairat

Monaco 0–0 Juventus

Bilbao 2–3 Sporting CP

Atlético 1–2 Bodø/Glimt

Leverkusen 3–0 Villarreal

Dortmund 0–2 Inter Milan

Club Brugge 3–0 Marseille

Frankfurt 0–2 Tottenham

Barcelona 4–1 Copenhagen

Liverpool 6–0 Qarabağ

Man City 2–0 Galatasaray

Pafos 4–1 Slavia Prague

PSG 1–1 Newcastle

PSV 1–2 Bayern

Union Saint-Gilloise 1–0 Atalanta

Benfica 4–2 Real Madrid

Napoli 2–3 Chelsea