KRC Genk Chuo cha soka kinachomwandaa Kelvin John

NI Ubelgiji Mashariki, karibu na mpaka wa Uholanzi ndipo yalipo maskani ya KRC Genk inayomwandaa mchezaji kinda wa Kitanzania, Kelvin John kama ambavyo ilikuwa kwa Thibaut Courtois na Kelvin De Bruyne ambao kwa sasa wanatesa Ulaya wakiwa na Real Madrid na Manchester City.

Umbali wa maili 100 kutoka Genk ni Brussels, Bruges, Antwerp na Liège, bila kusahau Rotterdam, Amsterdam, Eindhoven na Dortmund. Sio tu miji mikubwa, lakini iliyozama katika historia ya soka.

Licha ya KRC Genk kushuka daraja mara mbili kwenye historia yao, uamuzi wa kuunganisha Waterschei SV Thor Genk na KFC Winterslag ulithibitisha mafanikio na mwanzoni mwa karne, Genk walikuwa wameanza kufanya mapinduzi katika soka la Ubelgiji.

Walishinda taji hilo kwa mara ya kwanza 1998/99, wakirudia ujanja huo miaka mitatu baadaye.

Hiyo ilikuwa chachu ya kucheza mara ya kwanza katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na walipata sare dhidi ya vigogo wa Italia, Roma na mabingwa watetezi Real Madrid.

Hata hivyo, katika mazingira ya Ulaya, Genk ilikuwa kama samaki wadogo katika bwawa kubwa. Ili kupata nafasi yoyote ya kuwa na ushindani dhidi ya klabu kubwa kutoka kwenye ligi zenye nguvu zaidi zama za kisasa, wangehitaji kufanya kitu kisicho cha kawaida.

Ndio maana kuelewa hadithi ya Genk, hatua muhimu zaidi kwao sio taji ikitokea sio mbaya au kufanya makubwa kwenye Ligi ya Mabingwa badala yake nguvu zao kuanzia miaka ya 2000 waliwekeza kwa kiasi kikubwa katika miundombinu inayohitajika kuibua vipaji na sasa ni kama chuo kilichostawi.

Ulikuwa uamuzi makini, pamoja na imani isiyoyumba juu ya kuandaa nyota wa baadae, ambayo imetoa misingi ambayo imeiwezesha klabu kuwa na hadithi nzuri za kuvutia kwenye soka la Ulaya katika karne hii ya 21.

Kutoka kwa Kevin De Bruyne na Thibaut Courtois hadi Yannick Carrasco, Christian Benteke, Divock Origi na Leandro Trossard, orodha ya Genk ya wahitimu wa akademia ni ndefu ya kuvutia na inakua mara kwa mara.

Roland Breugelmans amekuwa sehemu ya safari hiyo tangu mwanzo. Kwa takriban miaka 35 kwenye klabu, ameona vipaji vyote vya vijana vya Genk vinavyong'aa zaidi na mara nyingi, wanaendelea kuangaza kwenye hatua kubwa zaidi.

Ingawa anasisitiza hakuna kichocheo cha siri ambacho mafanikio ya Genk yanaweza kuhusishwa nayo, Mkurugenzi wa Academy anaweza kuangazia mtazamo wao:

"Kwangu mimi, jambo muhimu zaidi unahitaji falsafa katika klabu yako, bodi inaamini kwa vijana. Tumekuwa tukitoa kwa kiasi kikubwa nafasi kwa vijana kwenye kikosi chetu.

"Tumekuwa na marais wengi, lakini kila rais anajua falsafa ya chuo chetu."

Historia ya hivi majuzi ya Genk imejaa visa vya wahitimu wa akademi kupata nafasi yao kwenye kikosi cha kwanza wakiwa na umri mdogo na kuchangamkia fursa  hiyo. Walakini njia ya umaarufu sio laini, hata kwa nyota wengine waliopita Genk kama Breugelmans anavyokumbuka,

“Thibaut alianza akiwa mvulana mdogo wa miaka minane. Hakuna mtu [angeamini] Thibaut ndiye huyu leo, kwangu, kipa bora zaidi duniani.

"Kevin ni hadithi nyingine. Kevin alikuwa na umri wa miaka 14, alitoka Gent. Hapo mwanzo, ugumu sio neno, lakini anahitaji wakati.

Courtois na De Bruyne walichanua na kuwa vijana wenye vipaji vya hali ya juu ambao waliisaidia Genk kushinda Ligi ya Ubelgiji ya 2010/11. Wote wawili walikuwa bado vijana tu wakati huo, lakini ushindi huo ungethibitisha mwisho wa muda wa Courtois kwenye klabu na uhamisho wa Chelsea majira ya joto, mara moja ikifuatiwa na miaka mitatu yenye mafanikio kwa mkopo huko Atlético Madrid.

De Bruyne pia alisaini Chelsea mapema mwaka uliofuata, lakini ilikuwa kwenye Bundesliga akiwa na Werder Bremen na Wolfsburg na alipiga hatua zinazofuata katika safari yake ya kuwa mmoja wa viungo wa kati bora kabisa.

"Tunahitaji pesa za kuuza wachezaji kwa sababu hatuna mtu mwenye pesa nyingi kama klabu za Uingereza," anaelezea Breugelmans.

"Kila mwaka tunatumai tunaweza kumuuza mchezaji, mfano wa Genk na Ubelgiji ni nchi ndogo na nadhani tunapenda kubaki pamoja  na wachezaji wetu wengi wazuri lakini haiwezekani kubaki na Onuachu wakati mezani kuwa Euro milioni 18,” anasema, akimrejelea mshambuliaji wa Nigeria, ambaye alifanya makubwa akiwa na klabu hiyo (ingawa sivyo mhitimu wa akademi) alitua Southampton.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Academy, Koen Daerden, mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Ubelgiji ambaye alikuwa mchezaji mchanga wa kikosi cha kwanza cha Genk mwenyewe wakati programu maarufu ya vijana ilipofunguliwa mwaka wa 2003, anaelezea kwa undani zaidi mbinu ya klabu.

"Tayari ni miaka 20. Ili kudumisha falsafa hii, utulivu huu. Hayo ndiyo mafanikio ya klabu yetu na kwa akademi,” anasema.

Juu ya mbinu ya ukuzaji wa wachezaji, Daerden anaelezea, "Yote ni juu ya kukuza na kuna mambo mengi karibu na mchezaji siku hizi. Sio tu kuhusu mpira wa miguu, pia kuhusu utu, ni kuhusu mazingira ya shule, lakini mazingira kwa jumla, mazingira ya kijamii.

"Tunapaswa kusimamia kila wakati, kila mchezaji ana kipaji au la, hata kama hayuko tayari leo, labda katika miaka michache ijayo.

"Kwa mfano, Leandro Trossard hakuwa tayari akiwa na umri wa miaka 17 au 18, lakini alifanya njia nyingine na kupitia njia hiyo akawa nyota ambaye yuko Arsenal sasa, lakini ilichukua muda mrefu zaidi ya Thibaut au hata Yannick (Carrasco) kwa hivyo kila mtu ana njia yake mwenyewe na kwa wakati fulani unaweza kusema hivi ndivyo au kwa nini walifanya hivyo, lakini ni juu ya chaguzi, kufanya chaguzi."

Kuna dalili ndogo ya mstari wa uzalishaji wa Genk kupungua. Wakati timu ya vijana chini ya umri wa miaka 19 ikifurahia mbio nzuri, ikiwaondoa Juventus na kutinga hatua ya 16 bora ya Ligi ya Vijana ya UEFA, timu ya wakubwa inaruka kileleni mwa Ligi ya Ubelgiji kabla ya hatua ya mchujo ikiwa na kipa mwenye umri wa miaka 21. Maarten Vandevoordt na kiungo wa kati Bilal El Khannous mwenye umri wa miaka 18 ni miongoni mwa wahitimu wa akademi wanaofanya vyema.

Vandevoordt tayari amekubali kujiunga na RB Leipzig ya Bundesliga mnamo 2024 na ndiye mchezaji mwenye kipaji ambaye anazungumzwa zaidi kwa sasa huku Kelvin akiendelea kupikwa huku ukisubiriwa mlango wake wa kutokea.

Mlinda mlango mdogo zaidi katika historia ya Ligi ya Mabingwa, Vandevoordt alikuwa na umri wa miaka 17 tu alipomenyana na Napoli katika hatua ya makundi ya 2019/20 na alikuwa amejiweka kama nambari moja wa Genk akiwa na umri wa miaka 18.

Uamuzi wa "kumchukua Maarten," kama Daerden anavyoweka, ulikuja wakati na vilabu vingi vingechukua chaguo salama zaidi kuleta kipa mwenye uzoefu zaidi.

Kupanda kwa Bilal El Khannous kumekuwa kwa kasi vile vile. Akiwa amecheza nafasi moja pekee ya timu ya wakubwa kabla ya msimu huu, chipukizi huyo mzaliwa wa Ubelgiji hajajiweka katika kikosi cha kwanza cha Genk, pia amefuatiliwa kwa kasi katika kikosi cha Morocco.

Hadithi yake pia inatoa mwanga wa falsafa ya Genk na baadhi ya njia wanazosimamia maendeleo ya wachezaji wachanga mbali na uwanja.

"Pia alipokea diploma yake kutoka shuleni. Alikuwa na nidhamu ya kuifanikisha yeye mwenyewe,” anaeleza Daerden. "Je, anaihitaji siku zijazo? Labda sivyo, lakini ni jambo ambalo sisi kama klabu pia tunawekeza—tazama, wavulana hawaachi shule kirahisi sana, hupati vitu peke yako, unahitaji kulifanyia kazi na shule ni jambo muhimu sana.

"Huwezi kujua baada ya miaka miwili, labda unajeruhiwa au kitu kama hicho kwa hivyo mambo hayo ni muhimu pia."

Baada ya muda, El Khannouss anaweza nyota anayefuata wa akademi ya Genk kuhamia ligi kubwa zaidi, lakini kupata wakati huo ni muhimu kwa pande zote.

"Wape pia fursa ya kwenda wanapokuwa tayari kwenda," anasema Daerden. "Unaweza kuona wachezaji wote wanaofanya uhamisho kwenda timu nyingine, wanacheza katika klabu yao kwa hiyo ina maana ni wakati mwafaka. Sio mapema sana, sio mapema sana.

"Tunafikiria zaidi kuliko KRC Genk pekee. Pia kama Thibaut, wao ni mabalozi, na sasa wachezaji wanaokuja, pia ni mabalozi. Tunawahitaji mabalozi hao pia kwa siku zijazo. Na inafanya kazi tu ikiwa mtafanya kazi pamoja kwa mustakabali wa mchezaji. Hilo ndilo lengo letu kuu pia."