KOMBE LA DUNIA QATAR 2022: Mziki mnene humu ndani

DOHA, QATAR. KUMEKUCHA. Timu 32 zitaonyeshana ubabe kwenye mechi 64, zitakazopigwa kwenye viwanja vinane. Bingwa mmoja tu.

Ni mwendo wa fainali za Kombe la Dunia 2022 zitakazopigwa huko Qatar, ambapo mziki wake utaanza rasmi Novemba 20 kwenye mechi ya ufunguzi na fainali yake itakuwa Desemba 18. Mchakamchaka wote huo utafanyika kwenye viwanja vya kibabe kabisa.

Viwanja mahususi kwa fainali za Kombe la Dunia 2022 huko Qatar ni Lusail Iconic uliopo Lusail, Al Bayt Stadium uliopo Al Khor, Al Janoub Stadium uliopo Al Wakrah, Ahmad Bin Ali Stadium, Khalifa International Stadium na Education City Stadium vilivyopo kwenye mji wa Al Rayyan na Stadium 974 na Al Thumama Stadium vinavyopatikana Doha. Viwanja vyote hivyo vimejengwa ndani ya eneo la kilomita 55 kuzunguka mji mkuu wa Qatar, Doha. Mwali wa Kombe la Dunia 2022 atasakwa humu.


LUSAIL STADIUM

Uwanja wa Taifa wa Lusail utatumika kwenye mechi 10 za Kombe la Dunia 2022, zikiwamo sita za makundi na nyingine za mtoano ikiwamo ya fainali. Mwonekano wa uwanja huo ni kama bakuli.

Uwezo: Watazamaji 80,000

Uzinduzi: 2022

Mechi zitakazopigwa

Novemba 22; Kundi C: Argentina v Saudi Arabia

Novemba 24; Kundi G: Brazil v Serbia

Novemba 26; Kundi C: Argentina v Mexico

Novemba 28; Kundi H: Ureno v Uruguay

Novemba 30; Kundi C: Saudi Arabia v Mexico

Desemba 2; Kundi G: Cameroon v Brazil

Desemba 5; 16 bora: 1H v 2G

Desemba 9; Robo fainali: W49 v W50

Desemba 13; Nusu fainali: W57 v W58

Desemba 18: Fainali


KHALIFA INTERNATIONAL

STADIUM

Uwanja wa Khalifa International utatumika kwenye mechi nane za Kombe la Dunia 2022, ikiwamo sita za hatua ya makundi, mechi moja ya hatua ya mtoano ya 16 bora na kipute kingine kitakachopigwa hapo ni cha kusaka mshindi wa tatu.

Uwezo: Watazamaji 40,000

Uzinduzi: 1976

Mechi zitakazopigwa

Novemba 21; Kundi B: England v Iran

Novemba 23; Kundi E: Ujerumani v Japan

Novemba 25; Kundi A: Uholanzi v Ecuador

Novemba 27; Kundi F: Croatia v Canada

Novemba 29; Kundi A: Ecuador v Senegal

Desemba 1; Kundi E: Japan v Hispania

Desemba 3; 16 bora: 1A v 2B

Desemba 17; Mshindi wa tatu.


STADIUM 974

Stadium 974 utatumika kwenye mechi saba za fainali za Kombe la Dunia 2022, sita za hatua ya makundi na moja ya mtoano kwenye hatua ya 16 bora. Uwanja huo umejengwa kwa makontena na vyuma ukiwa na mwenekano wa kipekee kabisa kwa mashabiki.

Uwezo: Watazamaji 40,000

Uzinduzi: 2021

Mechi zitakazopigwa

Novemba 22; Kundi C: Mexico v Poland

Novemba 24; Kundi H: Ureno v Ghana

Novemba 26; Kundi D: Ufaransa v Denmark

Novemba 28; Kundi G: Brazil v Uswisi

Novemba 30; Kundi H: Poland v Argentina

Desemba 1; Kundi G: Serbia v Uswisi

Desemba 5; 16 bora: 1G v 2H


AL BAYT STADIUM

Uwanja wa Al Bayt utatumika kwenye mechi tisa za Kombe la Dunia 2022, ikianzia ya ufunguzi na nyingine tano za hatua ya makundi na mechi tatu za hatua ya mtoano. Mwonekano wake ni kama mahema ukiwakilisha historia watu wa kuhamahama.

Uwezo: Watazamaji 60,000

Uzinduzi: 2021

Mechi zitakazopigwa

Novemba 20; Kundi A: Qatar v Ecuador

Novemba 23; Kundi F: Morocco v Senegal

Novemba 25; Kundi B: England v Marekani

Novemba 27; Kundi E: Hispania v Ujerumani

Novemba 29; Kundi A: Uholanzi v Qatar

Desemba 1; Kundi E: Costa Rica v Ujerumani

Desemba 4; 16 bora: 1B v 2A

Desemba 10; Robo fainali: W51 v W52

Desemba 14; Nusu fainali: W59 v W60


AHMAD BIN ALI STADIUM

Uwanja wa Ahmad bin Ali utatumika kwenye mechi saba za Kombe la Dunia 2022, sita za hatua ya makundi na moja kwenye hatua ya mtoano ya 16 bora. Uwanja huo umejengwa kwa dizaini za kibabe kabisa kuwakilisha utaduni na uzuri wa jangwani.

Uwezo: Watazamaji 40,000

Uzinduzi: 2020

Mechi zitakazopigwa

Novemba 21; Kundi B: Marekani v Wales

Novemba 23; Kundi F: Ubelgiji v Canada

Novemba 25; Kundi B: Wales v Iran

Novemba 27; Kundi B: Japan v Costa Rica

Novemba 29; Kundi B: Wales v England

Desemba 1; Kundi F: Croatia v Ubelgiji

Desemba 3; 16 bora: 1C v 2D


AL THUMAMA STADIUM

Uwanja wa Al Thumama utatumika kwenye mechi nane za fainali za Kombe la Dunia 2022 huko Qatar, ambapo mechi sita ni za hatua ya makundi na mbili zitakuwa za hatua ya mtoano. Dizaini inawakilisha baraghashia, kofia za kufuma kwa uzi za wanaume.

Uwezo: Watazamaji 40,000

Uzinduzi: 2021

Mechi zitakazopigwa

Novemba 21; Kundi A: Senegal v Uholanzi

Novemba 23; Kundi E: Hispania v Costa Rica

Novemba 25; Kundi A: Qatar v Senegal

Novemba 27; Kundi F: Ubelgiji v Morocco

Novemba 29; Kundi B: Iran v Marekani

Desemba 1; Kundi F: Canada v Morocco

Desemba 4; 16 bora: 1D v 2C

Desemba 10; Robo fainali: W55 v W57


AL JANOUB STADIUM

Uwanja wa Al Janoub utatumika kwenye mechi saba za fainali za Kombe la Dunia 2022, ambapo sita zitakuwa za hatua ya makundi na moja kwenye mtoano wa hatua ya 16 bora. Dizaini ya uwanja huo ni kuonyesha utamaduni wa majahazi.

Uwezo: Watazamaji 40,000

Uzinduzi: 2019

Mechi zitakazopigwa

Novemba 22; Kundi D: Ufaransa v Australia

Novemba 24; Kundi G: Uswisi v Cameroon

Novemba 26; Kundi F: Tunisia v Australia

Novemba 28; Kundi G: Cameroon v Serbia

Novemba 30; Kundi D: Australia v Denmark

Desemba 1; Kundi H: Ghana v Uruguay

Desemba 5; 16 bora: 1E v 2F


EDUCATION CITY

STADIUM

Uwanja wa Education City wenyewe utatumika kwenye mechi nane za fainali za Kombe la Dunia 2022 huko Qatar, ambapo sita zitakuwa za hatua ya makundi na mbili ni za mtoano. Umedizainiwa kuwakilisha almasi zinazopatikana Mashariki ya Kati.

Uwezo: Watazamaji 40,000

Uzinduzi: 2020

Mechi zitakazopigwa

Novemba 22; Kundi D: Denmark v Tunisia

Novemba 24; Kundi H: Uruguay v Korea Kusini

Novemba 26; Kundi C: Poland v Saudi Arabia

Novemba 28; Kundi H: Korea Kusini v Ghana

Novemba 30; Kundi D: Tunisia v Ufaransa

Desemba 2; Kundi H: Korea Kusini v Ureno

Desemba 6; 16 bora: 1F v 2E

Des 9; Robo fainali: W53 v W54.