Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kane: Tunataka kumaliza kazi mapema

KANE Pict
KANE Pict

Muktasari:

  • England itavaana na mabingwa watetezi Argentina kwenye mchezo wa nusu fainali ikitafuta nafasi ya kwenda fainali na kusaka ubingwa wao wa kwanza tangu mwaka 1966.

LOS ANGELES, MAREKANI: NAHIODHA Harry Kane amesema kizazi hiki cha England kimefika wakati wa kuandika historia kwa kutwaa ubingwa baada ya kufika hatua za mwisho mara kadhaa bila kubeba kombe.

England itavaana na mabingwa watetezi Argentina kwenye mchezo wa nusu fainali ikitafuta nafasi ya kwenda fainali na kusaka ubingwa wao wa kwanza tangu mwaka 1966.

“Hiki ni kipindi kizuri kwa timu yetu ya taifa, lakini bado tunahitaji kumaliza kazi. Hicho ndicho kipande kinachokosekana,” alisema mshambuliaji huyo wa Bayern Munich. Kane alikiri kuwa England bado haijafikia kiwango chake bora licha ya kufuzu nusu fainali.

KAN 01
KAN 01

“Kocha anajua uwezo tulionao. Anaamini tunaweza kucheza vizuri zaidi na sisi pia tunafahamu bado tuna kiwango kingine cha kuonyesha.”

England sasa itakutana na Argentina katika nusu fainali ya kusisimua itakayopigwa Jumatano, huku mshindi akitinga fainali ya Kombe la Dunia.