Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

FAI yaidhinisha azimio la kuzuia Israel kushiriki mashindano ya UEFA

FAI Pict

Muktasari:

  • Azimio hilo lililowasilishwa na klabu ya Bohemians yenye maskani yake mjini Dublin, linalenga kusitisha Israel kutokana na kuvunja vifungu viwili huru vya kanuni za UEFA. Upigaji kura ulimalizika kwa matokeo ya 74 dhidi ya 7, na sasa FAI itawasilisha ombi rasmi kwa mamlaka ya soka ya Ulaya kuhusu ukiukaji huo.

Mamlaka ya Mpira wa Miguu Jamhuri ya Ireland (FAI), imeidhinisha azimio linaloitaka Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA) kusitisha mpango wa klabu za Israel kushiriki mashindano ya bara hilo.

Azimio hilo lililowasilishwa na klabu ya Bohemians yenye maskani yake mjini Dublin, linalenga kusitisha Israel kutokana na kuvunja vifungu viwili huru vya kanuni za UEFA. Upigaji kura ulimalizika kwa matokeo ya 74 dhidi ya 7, na sasa FAI itawasilisha ombi rasmi kwa mamlaka ya soka ya Ulaya kuhusu ukiukaji huo.

Kuna ukaguzi mkubwa zaidi kuhusu ushiriki wa Israel katika soka la Ulaya tangu kuanza kwa vita Gaza. Zaidi ya Wapalestina 69,000 wameuawa na mashambulizi ya Israeli tangu shambulio la Hamas Oktoba 7, 2023, na Tume ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi ilikagua hali hiyo na kutoa hukumu kwamba Israel imefanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina, lakini Israel imepinga mashtaka hayo.

Hata hivyo, wachezaji walikusanyika Septemba 2025 kuomba Israel iondolewe kwenye mchakato wa kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2026 kutokana na vita. Oktoba 2025, FIFA iliamua kusitisha dhidi ya Israel, licha ya shinikizo la kimataifa.

FA 01

Azimio lililowasilishwa na Bohemians Jumamosi Novemba 8, 2025 lilisainiwa pia na klabu za Shamrock Rovers, Shelbourne, Cork City, chama cha wachezaji wa kulipwa nchini Ireland, na baadhi ya mashabiki na vyuo.

Ukiukaji uliotajwa katika azimio ni: "Kusimamia klabu kwenye maeneo yasiyo halali katika West Bank bila idhini ya Shirikisho la Soka la Palestina.

"Kutotekeleza na kusimamia sera madhubuti ya kupinga ubaguzi wa rangi."

Azimio hilo pia linaitaka UEFA kutoa vigezo vya uwazi kwa kusitisha au kuondoa mashirikisho ya wanachama ili kuhakikisha usawa kwa wote.

FA 02

Azimio hilo rasmi litawasilishwa UEFA na FIFA ili kuindoa Israel kushiriki soka la kimataifa. Ripoti zilizotolewa Septemba 2025, zilionyesha uwezekano wa kura ya UEFA, lakini mapatano ya amani kati ya Israel na Hamas yameathiri uwezekano huo.

Kwa mujibu wa Irish Times, FAI imesema: "Bodi ya Wakurugenzi ya FAI imeagizwa bila kuchelewa kuwasilisha azimio rasmi kwa kamati ya utekelezaji ya UEFA kuomba kusitishwa mara moja kwa Israel FA (IFA) kuondolewa kwenye mashindano ya UEFA kutokana na ukiukaji wa vifungu viwili huru vya kanuni za UEFA."

Kwa sasa, timu ya taifa ya Israel inashiriki kwenye mchakato wa kufuzu Kombe la Dunia, na Maccabi Tel Aviv inashiriki kwenye Europa League. Mchezo wao dhidi ya Aston Villa wiki hii ulikuwa gumzo, huku Waziri Mkuu Keir Starmer akikosoa uamuzi wa polisi wa West Midlands wa kuzuia mashabiki wao kutokana na usalama. 

FA 03

Marekani yapinga vikwazo
Kuanzishwa kwa vikwazo dhidi ya Israel kutafanya UEFA kuwa kinyume na serikali ya Marekani, inayopanga kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia 2026. Rais Donald Trump na utawala wake wameunga mkono Israel na wamepinga vikwazo vyote.

Jumamosi 2025, seneta wa Republican, Lindsey Graham alikosoa FAI kwa kuandaa kura hiyo, akisema Ireland italipa kwa kiasi kikubwa kwa kujaribu kuizuia Israel kushiriki michezo. 

"Ireland na wengine wangekuwa wanadhulumu watu wa Kiyahudi miaka 80 baada ya Holocaust (Kisa cha kihistoria cha mauaji ya kimbari na mateso makubwa yaliyofanywa na Nazi Ujerumani dhidi ya Wayahudi na makundi mengine wakati wa Vita Kuu ya Pili vya Dunia) kwa sababu wanapigana na makundi ya kigaidi yanayohitaji kuua Wayahudi wote. Hamas alianza vita hii. Hamas imeweka raia katika hatari ili kuendeleza vita hii. Na Hamas ni kundi la kigaidi la Kiislamu lililoazimia kuharibu Israel. Lazima waishinde kisiasa na kiasasi."

Ameongeza: "Iwapo mashambulizi dhidi ya Israel yataendelea, nitafanya kila niwezalo kuhakikisha washiriki wote wa juhudi za kuiondoa Israel michezoni, na sehemu nyingine, walipwe gharama kubwa ikiwemo upatikanaji wa uchumi wa Marekani."