Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Aston Villa yamtoa machozi mwanamfalme William

WILLIUM Pict

Muktasari:

  • Mwanamfalme huyo alinaswa kwenye video akishangilia kwa hisia kali, akimkumbatia kocha wa Aston Villa, Unai Emery, na kusherehekea kwa karibu kabisa na mashabiki wengine jukwaani.

ISTANBUL, UTURUKI: MWANAMFALME William amejumuika katika sherehe za kihistoria baada ya klabu anayoishabikia ya Aston Villa kutwaa ubingwa wa Europa League kufuatia ushindi mnono wa mabao 3-0 nchini Uturuki. 

William mwenye umri wa miaka 43, alionekana mwenye furaha tele huko Beşiktaş Park mjini Istanbul, huku ushindi huo ukimaliza ukame wa mataji ya Ulaya uliokuwa nao klabu hiyo uliodumu kwa miaka 44 tangu ilipotwaa mara ya mwisho. 

Mwanamfalme huyo alinaswa kwenye video akishangilia kwa hisia kali, akimkumbatia kocha wa Aston Villa, Unai Emery, na kusherehekea kwa karibu kabisa na mashabiki wengine jukwaani.

WILL 03

Kupitia video zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii, William alionekana akiimba kwa hisia nyimbo maarufu za ushindi za "Sweet Caroline" na "We Are the Champions" huku akitokwa na machozi ya furaha wakati wachezaji wakinyanyua kombe.
 
Baada ya filimbi ya mwisho katika fainali hiyo dhidi ya Freiburg iliyochezwa usiku wa Jumatano ya Mei 20, 2026, William alitumia simu yake ya mkononi kurekodi matukio hayo ya kihistoria na kisha kuchapisha ujumbe wa pongezi mtandaoni akisema: "Villa 'Til I Die". 

WILL 01

Katika ujumbe huo, alimpongeza kiungo Boubacar Kamara ambaye amekuwa nje kwa majeraha, akitambua mchango wake mkubwa ulioweka misingi ya mafanikio hayo.

WILL 02

Hali ya hewa ilizidi kunoga baada ya mechi hiyo pale nahodha wa Aston Villa, John McGinn, alipotania mbele ya waandishi wa habari kuwa wanatumai Mwanamfalme huyo atagharamia vinywaji vyao usiku huo. 

McGinn alimsifu William kwa kuwa mtu wa kawaida na mnyenyekevu, akifichua kuwa alitembelea vyumba vya kubadilishia nguo kabla ya mechi kutoa hamasa. 

Ushindi huo umeweka historia mpya kwa Aston Villa na kuacha kumbukumbu isiyofutika kwa mashabiki wote, akiwemo Prince William.