Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Arteta atoa msimamo wa beki Saliba

SALIBA Pict

Muktasari:

  • Saliba bado ana hatihati ya kuwamo uwanjani kwenye mechi ya Jumamosi dhidi ya Wolves kwenye Ligi Kuu England, sawa na mastaa wengine kama Declan Rice, Leandro Trossard na Jurrien Timber.

LONDON, ENGLAND: KOCHA, Mikel Arteta amefunguka juu ya hali ya kiafya ya beki wa kati wa Arsenal, William Saliba.

Beki huyo wa kati wa Arsenal alipata maumivu ya enka na kukosa mechi nne za mwisho za miamba hiyo ya Emirates.

Saliba bado ana hatihati ya kuwamo uwanjani kwenye mechi ya Jumamosi dhidi ya Wolves kwenye Ligi Kuu England, sawa na mastaa wengine kama Declan Rice, Leandro Trossard na Jurrien Timber.

Alipoulizwa kuhusu Saliba, Arteta, ambaye mara zote amekuwa wakilalamika kuhusu mastaa wake kuwa majeruhi, amesema: “Ngoja tusubiri tuone. Jana hakufanya mazoezi, hajafanya mazoezi na sisi. Ngoja tuone, kama atakuwapo au la.

“Kama utaniuliza kuhusu mechi ya Everton, nadhani atakuwa fiti. Kwa mechi ya Jumamosi, sifahamu.”

Timber aliumia kwenye mechi ya kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Aston Villa na alikosa mechi ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Club Brugge kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyofanyika Jumatano iliyopita.

Alipoulizwa kuhusu Mdachi huyo, Arteta amesema: “Itategemea hali itakavyokuwa. Aligongwa na hakuwa akijisikia vizuri. Nadhani ni suala la muda. Kama atacheza mechi hii au la, ngoja tuone.”

Kiungo ghali, Rice hakusafiri na timu hiyo ilipokwenda Ubelgiji kutokana na kuwa mgonjwa na kocha Arteta alibainisha naye ni mchezaji wanayesikilizia kuhusu hali yake. Kocha huyo Mhispaniola, amekuwa na wasiwasi pia na Trossard, ambaye amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya kigimbi.


MECHI ZA LIGI KUU ENGLAND WIKIENDI HII

Desemba 13, 2025

Chelsea           v Everton

Liverpool v Brighton

Burnley v Fulham

Arsenal v Wolves


Desemba 14, 2025

Crystal Palace v Man City

Nottm Forest v Tottenham

Sunderland v Newcastle

West Ham v Aston Villa

Brentford v Leeds United


Desemba 15, 2025

Man United v Bournemouth