Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Watatu waliotemwa Simba wapata dili

NYOTA watatu kati ya sita waliotemwa na Simba katika dirisha dogo, Nassor Kapama, Jimmyson Mwanuke na Shaaban Idd Chilunda wamepata dili baada ya kunaswa na Mtibwa Sugar na KMC.

Mwanuke na Kapama wametua zao Mtibwa, wakati Chilunda aliyewahi kuwika na Azam FC akisajiliwa KMC ili kuendeleza moto alioshindwa kuuwasha Msimbazi.

Akizungumza na Mwanaspoti, Kapama alisema ni kweli amemalizana na Mtibwa kwa mkataba wa miezi sita baada ya kuvunjiwa mkataba na Simba sasa atakuwa huko kuipambania timu hiyo isishuke daraja.

“Nimemalizana na Mtibwa nitacheza huko kwa miezi sita naamini ni chaguo sahihi baada ya ofa nyingi nilizokuwa nazo naamini nitapambana kwa kushirikiana na wenzangu ili kuiondoa timu hiyo kwenye hatari ya kushuka daraja.” alisema Kapana.

Wakati huohuo rafiki wa karibu wa Mwanuke ameliambia gazeti hili kuwa beki huyo amejiunga na Mtibwa kwa mkopo akitokea Simba.

“Mwanuke ametolewa kwa mkopo na Simba ili aweze kuisaidia Mtibwa kukwepa janga la kushuka daraja kutokana na kuwa katika nafasi mbaya,” kilisema chanzo.