Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO: Tshishimbi: Tumevuna tulichopanda kwa Morrison

Muktasari:

Tshishimbi amesema ubora wao mkubwa katika safu yao ya ushambuliaji ulitakiwa kutokana na ubora wa Morrison lakini hakuwa katika ubora.

Nahodha wa Yanga Papy Tshishimbi amesema matukio ya kucheza katika kiwango duni kwa mshambuliaji wao Bernard Morrison ni makosa ambayo yametokana na mapungufu ya aina mbili.

Tshishimbi amesema ubora wao mkubwa katika safu yao ya ushambuliaji ulitakiwa kutokana na ubora wa Morrison lakini hakuwa katika ubora.

Tshishimbi amesema Morrison hakuwa sawa kucheza kwa muda mrefu mchezo huo wa jana wa Nusu Fainali ya Kombe la Azam Shirikisho.

"Morrison hakuwa sawa,ukiangalia mchezo wa Kagera kitu pekee bora alichofanya ni kufunga lile bao lakini ukiangalia anavyocheza utagundua hakuwa sawa" amesema Tshishimbi.

"Jana Morrison hakuwa fiti,hakusaidia majukumu mengi ya timu ni wakati wa makocha kujifunza kupitia makosa ya kumfanya acheze.

Aidha Tshishimbi amesema mbali na makocha pia viongozi wa klabu hiyo wanatakiwa kuangalia jinsi ya makosa ya Morrison.

"Morrison hata nidhamu yake haikuwa sawa,unapokuwa unacheza mchezo mkubwa kama huu kuna heshima unayotakiwa kuonyesha.

"Viongozi wanatakiwa kujifunza jinsi ya kuishi na mchezaji husika,wanatakiwa kuangalia wamekosea wapi."