Twite aziba nafasi ya Kessy

Hassan Kessy
Muktasari:
JUHUDI Za Yanga kumtumia Hassan Kessy katika mechi yao ya usiku huu dhidi ya MO Bejaia, zimekwama na Kocha Hans Pluijm amemuanzisha Mbuyu Twite katika beki ya kulia.
JUHUDI Za Yanga kumtumia Hassan Kessy katika mechi yao ya usiku huu dhidi ya MO Bejaia, zimekwama na Kocha Hans Pluijm amemuanzisha Mbuyu Twite katika beki ya kulia.
Awali kulikuwa na dalili zote za Kessy aliyetua Jangwani kutoka Simba kukipiga katika mechi ya leo, lakini kucheleweshwa kwa jina lake kutoka CAF limemzuia kukipiga katika pambano hilo litakalochezwa kuanzia saa 6:15 usiku.
Kikosi kamili cha Yanga katika mchezo huo kipo hivi:
Deo Munishi 'Dida', Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Vincent Bossou, Thabani Kamusoko, Dues Kaseke, Haruna Niyonzima, Donald Ngoma, Simon Msuva na Amissi Tambwe.