Oscar Joshua afunga ndoa

Muktasari:
- Oscar amefunga ndoa hiyo na mchumba wake wa siku nyingi, ambaye pia ni mama wa watoto wake wawili.
Beki wa kushoto wa zamani wa Yanga, Oscar Joshua amefunga ndoa na mkewe, Monica katika kanisa la TAG jijini Mwanza jana Jumamosi.
Oscar amefunga ndoa hiyo na mchumba wake wa siku nyingi, ambaye pia ni mama wa watoto wake wawili.
Baada ya ndoa hiyo jijini Mwanza, Oscar anatarajia kufanya sherehe nyingine jijini Dar es Salaam.
"Nashukuru nimekamilisha suala la ndoa hii na sasa narudi kufanya mambo mengine hasa uwanjani ambako nilisimama kwa muda,"alisema Oscar.