Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ntibazonkiza apewa Prisons

SUPASTAA Saidi Ntibazonkiza amepewa shavu la kuanza kwenye kikosi cha kwanza cha Simba ambacho muda mchache ujao kitacheza dhidi ya Mafaande wa Tanzania Prisons kwa Mkapa.

Nyota huyo ambaye amejiunga na Simba akitokea Geita Gold  kwa mkataba wa miaka miwili wakati wa dirisha hili la usajili hii itakuwa mara yake ya kwanza kuwatumikia wekundu hao wa Msimbazi.

Licha ya ugeni wake, kocha wa Simba, Juma Mgunda ameamua kumtishwa mabomu mshambuliaji huyo ili aongoze safu yake sambamba na John Bocco.

Ntibazonkiza ambaye aliwahi kuichezea Yanga kabla ya kwenda Geita  anatazamwa kama mchezaji ambaye anaweza kuongeza makali kwenye safu hiyo ya ushambuliaji kutokana na kukosekana kwa Moses Phiri ambaye ni majeruhi.

Kikosi kamili cha Simba kinaundwa na Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein 'Tshabalala', Joash Onyango, Hennock Inonga, Sadio Kanoute, Clatous Chama, Mzamiru Yassin, Bocco, Ntibazonkiza na Pape Sakho.