Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Njia ya Jangwani yafungwa, Simba ikijiandaa kuwakera watani wao

NJIA Pict

Muktasari:


  • Kwa mujibu wa ratiba ya awali, msafara wa Simba ulipaswa kupita Jangwani kabla ya kuelekea Msimbazi na baadaye kuhitimisha shamrashamra zake katika fukwe za Coco.

WAKATI msafara wa Simba wa kusherehekea ubingwa wa Kombe la Shirikisho la CRDB ukiendelea katika mitaa mbalimbali ya Dar es Salaam, bado haijajulikana utakavyopita eneo la Jangwani baada ya njia hiyo kufungwa.

Kwa mujibu wa ratiba ya awali, msafara wa Simba ulipaswa kupita Jangwani kabla ya kuelekea Msimbazi na baadaye kuhitimisha shamrashamra zake katika fukwe za Coco.

NJI 03

Hata hivyo, taarifa kutoka eneo hilo zinabainisha kuwa barabara ya Jangwani imefungwa kufuatia shughuli za Yanga, ambayo jana, Jumamosi, ilifanya paredi ya kusherehekea ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC. 

NJI 01

Katika paredi hiyo, Yanga ilianzia Karume, ikapita Msimbazi kabla ya kuhitimisha msafara wao Jangwani.

Kutokana na hali hiyo, bado kuna sintofahamu kuhusu namna msafara wa Simba utakavyopita pindi utakapofika eneo la Jangwani huku mashabiki wakisubiri kuona kama utaruhusiwa kuendelea kama ilivyopangwa au waandaaji na vyombo vya usalama wataelekeza kutumia njia mbadala.

NJI 02

Mpaka sasa, hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu mabadiliko yoyote ya ratiba ya msafara huo huku wengi wakisubiri kuona nini kitatokea mara baada ya msafara wa Simba utakapowasili hapo.