Ninja ni Yanga tu
Muktasari:
HUU mfumo wa uchezaji wa Yanga hasa inapocheza na Simba SC huwa ni kujilinda zaidi na kufanya mashambulizi machache ya kushtukiza hivyo lazima Wekundu wa Msimbazi wafanye sana kazi ili washinde mechi zao.
Marlow kichwa kingine
YAANI huyu Marlaw ni bonge la msanii ila sijui imekuwaje. Tatizo la Watanzania ni U-Ali Kiba na U-Diamond ndiyo unapelekea hata huyu jamaa asisikike au asiongelewe kabisa ila kwa wanaomjua Marlaw kazi zake si mchezo na zinakubalika kama ninavyozikubali mimi.
Rashid Ramadhan
Ninja ni Yanga tu
ABDALLAH Shaibu ‘Ninja’ anastahili kucheza Yanga tu lakini si kwa Simba maana staili yake ya kucheza haifanani na kimataifa kabisa bali Yanga. Anabutua butua tu mipira, alipigwa chenga moja hatari sana na Zana Coulibaly mpaka akakaa, alishindwa kuzuia krosi ya kuchopu ya nahodha wa Simba, John Bocco.
Rashid Kitiku
Yanga noma
HAKUNA kuogopa Yanga ni Yanga tu, tupo pamoja wadau kazi ni moja tu kuhakikisha tunazidi kushinda.
Saddam Lubida
Kama tulikuwa wote
MWANDISHI aliyemkumbuka Marlow namshukuru sana kwa kuniulizia maswali haya ambayo hata mimi nimekuwa najiuliza mara nyingi yaani ni kama ulikuwa na mimi. Kwa hili hapa nafikiri tutapata majibu sahihi kuhusu Marlow.
Zacharia Lughano
Beki hasifiwi
Beki Abdallah Shaibu ni jembe haswa. Hayo mambo ya fujo nani kakwambia beki anasifiwa, huwa hasifiwi. Hongera kwake Ninja jamaa kama Sergio Ramos kwani ukienda kizembe anakufyatua tu.
Fred Clement
Yondani umezingua
KITENDO cha Ibrahim Ajibu kuwashika mikono wachezaji wenzake kweli si sawa lakini pia isingekuwa jambo la jinai kama Kelvin Yondani ‘Vidic’ angempa mkono mwenzake.
Ikupilika Sakuka
Kuifunga Yanga kazi
HUU mfumo wa uchezaji wa Yanga hasa inapocheza na Simba SC huwa ni kujilinda zaidi na kufanya mashambulizi machache ya kushtukiza hivyo lazima Wekundu wa Msimbazi wafanye sana kazi ili washinde mechi zao.
Rashid Kitiku
Zahera profesheno
KOCHA wa Yanga Mwinyi Zahera ameonyesha kuwa ni profesheno kwenye soka baada ya kukubali kuwa Simba iliwazidi kiwango, safi sana. Hii si kama hawa rafiki zangu wengine wanaojifanya mashabiki kindakindaki kelele tupu.
Jumaa Farijallar
Mkongo si mnafiki
HIVI kwa nini Mwinyi Zahera asiukubali mziki wa Simba kwa sababu Kwann huyu kocha si mnafiki anasema ukweli ingawa wakati mwingine kauli zake hizo za kusema ukweli zinaweza kumweka matatani.
Must Swaleh Kongowea