Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Manji atua, apagawisha wanachama mkutano Yanga

Muktasari:

Ujio wa Yanga wanachama walianza kuimba jina lake nje ya ukumbi mpaka ndani.

MWENYEKITI wa zamani wa klabu ya Yanga, Yusuph Manji ameteka mkutano baada ya kuwasili katika ukumbi wa DYCC jijini Dar es Salaam kwenye mkutano mkuu wa klabu hiyo.

Manji aliwasili saa 11:07 asubuhi akiongozana na gari mbili, moja aina ya Nissan Xtrail na nyingine Toyota Land Cruiser.

Baada ya gari hizo kuwasili wanachama walikuwa hawajui yupo katika gari gani lakini Manji alishuka kwenye Nissan Xtrail na wanachama wakaanza kupiga shangwe.

Wanachama walimfungulia mlango na wakaanza kupiga nae picha huku yeye mwenyewe akionyesha kufurahi.

Manji alitoa nafasi kwa kila mwanachama aliyekuwa nje kupiga nae picha lakini makomandoo ndio walikuwa wanakataa.

Baada ya kumaliza kupiga picha na baadhi ya wanachama, Manji aliingia ndani na alianza kushangiliwa.