Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Lyanga, Mahadhi kuongoza jeshi la Geita

KOCHA Etiene Ndayiragije wa Geita Gold amewaanzisha washambuliaji Juma Mahadhi na Daniel Lyanga katika eneo la ushambuliaji kwenye mchezo dhidi ya Yanga utakaochezwa saa 1:00 usiku leo kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.

Lyanga ni miongoni mwa washambuliaji hatari na msimu uliopita akiwa na JKT Tanzania aliifungia timu hiyo mabao tisa, huku upande wa Mahadhi yeye alipokuwa na Ihefu ni kama alikuwa anarejea kwenye ubora wake baada ya kukaa nje kwa muda mrefu kisa majeraha.

Kwenye kikosi hicho pia kiungo Maka Edward ambaye alishacheza Yanga na soka la kulipwa nchini Morocco katika klabu ya Moghreb Toutan na msimu huu amerejea tena nchini.

Pia katika upande wa beki yupo Oscar Masai ambaye msimu uliopita aliichezea timu ya Ihefu Fc ambayo imeshuka daraja.

Kikosi kilichoanza ni Khomeinh Abubakar, Derick Mussa, Amosi Kidikilo, Chilo Mkama, Oscar Masai, Yusph Kagoma, Kalagha Mbindo.

Wengine ni Raymond Massota, Daniel Lyanga, Maka Edward na Juma Mahadhi.