Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

KVZ yaizima Malindi, ikiingia vita ya ubingwa

KVZ Pict

Muktasari:

  • Ushindi huo uliopatikana kwenye Uwanja wa Mao A umeifanya KVZ kufikisha pointi 47, moja pungufu na ilizonazo Mafunzo inayoongoza msimamo ambayo nayo jana ilibanwa mbavu na Zimamoto kwa kutoka suluhu katika mechi nyingine ya ligi hiyo.

MAAFANDE wa KVZ jana imeizima Malindi kwa mabao 2-1 na kuchupa hadi nafasi ya pili kutoka ya nne ikiingia katika vita ya ubingwa wa Ligi Kuu Zanzibar (ZPL).

Ushindi huo uliopatikana kwenye Uwanja wa Mao A umeifanya KVZ kufikisha pointi 47, moja pungufu na ilizonazo Mafunzo inayoongoza msimamo ambayo nayo jana ilibanwa mbavu na Zimamoto kwa kutoka suluhu katika mechi nyingine ya ligi hiyo.

Michael Joseph aliitanguliza  KVZ kwa  bao la dakika ya 23 kabla ya mchezaji huyo kuongeza la pili dakika ya 38 na kufanya hadi mapumziko maafande hai wawe mbele kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili timu zote ziliungia na nguvu na hasa baada ya mabadiliko kadhaa ya wachezaji na Malindi kunufaika kwa kupata bao la kufutia machozi.

Katika mechi nyingine ya Ligi hiyo, Mafunzo na Zimamoto zilitoka suluhu kwa kutofungana Uwanja wa Mao B, huku JKU ikikumbana na kipigo cha 2-1 kutika kwa Junguni United kwenye Uwanja wa FFU Finya  kisiwani Pemba.

Andrea James wa Junguni aliweka kimiani bao la kwanza dakika ya tano kabla ya Fredy Suleiman kuisawazishia JKU ambao ni watetezi wa ZPL dakika ya 55 na  Chawaka alipachika bao la pili katika dakika 90+3 za nyongeza.

Ligi hiyo itaendelea leo jioni kwa Mlandege kuvaana na Tekeleza kwenye Uwanja wa  Mao A. Tekeleza tayari imeshashuka daraja na msimu ujao itacheza daraja la kwanza, huku Uhamiaji itachuana na Mwenge Uwanja wa Mao B na Chipukizi watakutana na Mwembe Makumbi kwenye Uwanja wa Finya, Pemba.