Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kundi la Tip Top Connection lasambaratika

Muktasari:

  • Kundi hilo linasimamiwa na Meneja wao Babu Tale  ambaye pia anamsimamia mwanamuziki Diamond Patnum.

Msanii Tunda Man amesema  kundi la Tip Top Connection limesambaratika ambapo kila mtu anafanya  kazi kivyake.

Miaka kadhaa inakatika hakuna kazi za pamoja  kwa wasanii ambao wanaunda  za hilo 'Tip Top Connection' linaloundwa na Dogo Janja, Madee na Tunda Man.

Kundi hilo linasimamiwa na Meneja wao Babu Tale  ambaye pia anamsimamia mwanamuziki Diamond Patnum

Tunda aliweka bayana baada ya kuulizwa na MCL Digital akisema, "Daah kitambo kundi limevunjika na ndio maana unaona sasa hivi kila mmoja anatoka kivyake, ila katika maisha ya kawaida tuko pamoja na tunasaidiana mmoja wetu akitoa kazi.

 

"Na sio haja ya kuendelea kuficha wakati wazi mashabiki zetu wanajua kabisa, sio kawaida yetu kukaa kimya bila ya kutoa kazi mpya katika kundi letu, na wasitegemee kama linaweza kurudi hili kundi."

Tip Top Connection ni kundi lililokuwa  maskani yake Manzese, liliwahi kutamba na nyimbo kama, 'Bado tunapanda' 'Riziki' Goma la Manzese na nyingine nyingi.