Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kumbe Shikhalo ndiye kamvuta Aucho Yanga

Yanga imshukuru kipa Mkenya ambaye uhakika wataachana naye Faruk Shikhalo anayekubalika na mashabiki wa timu hiyo, Mwanaspoti linafahamu kwamba kiungo wa kimataifa wa Uganda, Khalid Aucho alibaki kidogo asisaini Yanga ili atue Simba.

Kiungo huyo kabla ya kufanya maamuzi yoyote aliwasiliana na kipa huyo kisha akataka kujua kama Yanga inalipa wachezaji kwa wakati akiambiwa kwamba timu hiyo hailipi vizuri.

Hata hivyo majibu ya Shikhalo yalimaliza kila kitu akimwambia mpaka wanamaliza mechi ya mwisho hakukuwa na madai yao yoyote na kwamba hawajawahi kucheleweshewa malipo.

Majibu hayo yalimsukuma kiungo huyo kujaa katika 18 za mabosi wa Yanga akiwaambia kwamba anakuja baada ya kujiridhisha,