Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kipigo cha Yanga, chatimua makocha Simba

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Saa chache tu tangu ipokee kipigo cha mabao 5-1 kutoka kwa Yanga, mabosi wa klabu ya Simba leo Novemba 7 imefikia makubaliano ya kuachana na Kocha Roberto Oliveira 'Robertinho' na kocha wa viungo Corneille Hategekimana.

Taarifa kutoka klabu hiyo inasema "Simba imefikia makubaliano ya pande zote mbili ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza cha Simba, Roberto Oliveira (Robertinho) na kocha wa viungo, Corneille Hategekimana”.

“Uongozi wa klabu ya Simba unawashukuru makocha hawa kwa mchango wa ndani ya klabu yetu na inawatakia kila la heri katika majukumu yao mapya.”

Timu hiyo itakuwa chini ya kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Selemani Matola huku mchakato wa kutafuta makocha wapya ukiendelea.