Karume yafunika, mashabiki wapagawa

Muktasari:
- Yanga imewasili Karume 16:00 na kusababisha msongamano wa watu barabarani huku magari yakishindwa kuendelea na safari.
PAREDI la Yanga limeibua shangwe saa chache baada ya kuingia mtaa wa Karume shangwe na ongezeko la mashabiki wakiusindikiza msafara limetawala.
Yanga imewasili Karume 16:00 na kusababisha msongamano wa watu barabarani huku magari yakishindwa kuendelea na safari.
Gari hiyo iliyobeba wachezaji, viongozi na mataji ya timu hiyo msimu huu ilisimama kwa muda Karume na kuwapungia mikono baadhi ya mashabuki waliokuwa juu ya soko la ghorofa ambao waliibua shangwe.
Ukiondoa mashabiki waliojisogeza kando ya barabara wananchi wanaoishi maeneo hayo pia wamesimama madirishani na kuchukua picha gari ya paredi.
Kituo cha Mwendokasi cha Machinga Complex kimegeuka ukingo wa mashabiki kusimama kushuhudia paredi huku wafanyabiashara wadogo wadogo wakisitisha kazi kwa muda kuwashangilia wachezaji huku wakiwataja watani zao Simba kuwa hawana nafasi zaidi ya misimu kumi watatawala wao.
Yanga inafanya paredi kusherehekea makombe yake matano iliyotwaa msimu huu, imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara, Kombe la Shirikisho la CRDB, Kombe la Toyota, Ngao ya Jamii na Kombe la Muungano.