Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kaluwa: Nitatoa ushirikiano kwa kila mmoja wetu

New Content Item (1)
New Content Item (1)

ALIYEKUWA mgombea wa nafasi ya Uenyekiti wa Klabu ya Simba, Moses Kaluwa amesema ataendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wenzake licha ya kushindwa na mpinzani wake, Murtaza Mangungu.

Kaluwa amezungumza hayo ikiwa ni muda mchache tangu kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi na Mwenyekiti wa Kamati hiyo iliyokuwa inasimamia shughuli hiyo, Boniface Lihamwike.

"Nichukue nafasi hii kuwashukuru kwa wale wote walionipa kura zao, Simba ni kubwa kuliko mtu yeyote hivyo niseme wazi kwamba nitashirikiana na viongozi wote waliokuwa madarakani."

Katika uchaguzi huo ambao matokeo yake yametangazwa Afajiri ya Januari 30, Kaluwa amepata kura 1,045 huku Mangungu ambaye alikuwa anatetea kiti chake akipata jumla ya kura 1,311.