Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Huku Kipre, kule Molia Azam ya moto


AZAM imemaliza msimu wa 2025-2026 bila kupata kombe lolote hatua ambayo imewatibua matajiri wa klabu hiyo na sasa mpango wa msimu ujao unatishia.


Azam imeshamalizana na wachezaji watatu wa kigeni wakiwemo mawinga wawili ambao ndio balaa litakakapokuwepo kwa timu pinzani na namna ya kuwatuliza.

Azam imeshamalizana na winga Henoc Molia kutoka FC Lupopo ambaye ameshasaini mkataba wa miaka miwili kisha kurudi kwao DR Congo kujiandaa na maisha mapya na matajiri hao wa Chamazi.

Molia kwasasa ndiye winga bora Ligi Kuu ya DR Congo, msimu uliopita amefanya balaa zito akihusika kwenye jumla ya mabao 15.

Molia anajua kufungua ukuta wa wapinzani na kufunga, ambapo winga huyo ni chaguo la kwanza la kocha Florent Ibenge ambaye anataka kujenga timu yenye ubora wa kutengeneza mashambulizi.

Achana na Molia ambaye anaweza kushambulia akitokea kulia, balaa lingine la Azam ni kurejea kwa Kipre Junior ambaye aliuzwa MC Alger.

Azam inamrudisha Kipre nchini baada ya kufikia makubaliano na Waarabu hao wa Algeria akija kurudisha ubora ambao aliuacha misimu miwili iliyopita.

Kipre atakuwa uhakika na winga moja pale kwenye kikosi cha Azam akigawana na Molia wote wakiwa na ubora wa kujua kufungua ukuta wa wapinzani.


MSIKIE IBENGE

Akizungumza na Mwanaspoti mapema kabla ya msimu kumalizika, Ibenge alisema wanataka kujenga timu imara zaidi itakayoweza kutengeneza mashambulizi na kuyatumia kwa msimu ujao.

Ibenge alisema kwenye usajili wao wa msimu ujao wataleta wachezaji wenye ubora mkubwa ambao watakuja kuiongezea nguvu Azam tofauti na ilivyokuwa msimu uliomalizika.

"Usajili haujawahi kumalizika, unapomaliza kujenga hapa utahitaji kuimarisha sehemu nyingine, kwa msimu ujao ni kweli tutaleta wachezaji bora zaidi tunataka kuwa na timu imara zaidi," alisema Ibenge.

"Wakati mwingine usajili ni kama kamiri lakini ukweli ni kwamba tumeanza mchakato wa kutafuta wachezaji bora sana ambao watakuja kutupa kitu kikubwa zaidi ya hiki ambacho tumekipata msimu huu."