Horseed yairudisha Azam Chamazi
Mchezo wa marudiano kati ya Azam na Horseed katika kombe la Shirikisho barani Afrika uatakaopigwa Jumamosi Septemba 18 umerudishwa katika uwanja wa Azam Complex badala ya Uhuru.
Akizungumza Ofisa Habari wa Azam, Thabit Zakaria amesema Horseed wameamua kuamisha mchezo huo kutoka Uhuru hadi Azam Complex baada ya kufurahi miundombinu iliyopo uwanjani hapo
“Horseed wameamua kuamisha mechi yetu Azam Complex baada ya mechi yetu ya awali kupangwa kuchezwa Uhuru na sababu kubwa ni wao kuridhishwa na miundombinu iliyopo Chamazi” anasema Zakaria
Mechi ya kwanza Azam ilishinda mabao 3-1 wakiwa wenyeji wa mechi hiyo.
IMEANDIKWA NA LILIAN MUKULU